Type Here to Get Search Results !

SIMULIZI YA KIJASUSI: PENIELA SEHEMU YA 16 HADI 20



🔥🌹
SEASON 1
SEHEMU YA 16
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ Tafadhali usilie Penny.Usilie malaika wangu.Kuna mambo mengi ambayo yametokea kitu cha kwanza ninachokihitaji toka kwako ni msamaha wako.Ni kweli nilikuacha ukaingia katika matatizo makubwa na sikusimama pamoja nawe.Penny please forgive me my angel.We have so many to talk” akasema Dr Joshua.Penny akainua kichwa akamtazama na kusema
“ Nimekwisha kusamehe Dr Joshua na ndiyo maana niko hapa.Umesema tuna mambo mengi ya kuongea hata mimi nina mengi ya kuuliza lakini kwanza nataka unieleze kwa nini Edson aliuawa? Akauliza Penny.Dr Joshua akachukua kitambaa na kujifuta jasho,akainuka na kwenda mezani akajimiminia mvinyo na kupiga funda kubwa.
ENDELEA………………………………….
“ Kwa nini unataka kufahamu Penny? Akauliza Dr Joshua
“ Edson was my friend and my lover so I need to know why you ordered him killed” akasema Penny
“ He was your lover ! akasema Dr Joshua kwa sauti ya juu.Penny hakujibu kitu akakaa kimya
“ You cheated on me !
“ I loved him..He was such a gentleman” akasema Penny na Dr Joshua akakaa kimya akazunguka chumbani halafu akasema
“ Unataka kuufahamu ukweli?
“ Ndiyo nahitaji kuufahamu ukweli “ akasema Penny.Dr Joshua akamsogelea akamshika mkono na kusema
“ Ni wivu ndio ulionifanya nitoe maamuzi yale.Ninakupenda mno Peniela na nilipogundua kwamba unanisaliti kwa kutembea na Yule kijana nilikasirika sana.Penny wewe ni wangu peke yangu na sitaki unichanganye na mtu yeyote hususani hawa vijana wadogo.Kijana Yule hakuwa na kitu chochote cha kukupatia .Nilikuahidi kukupa kila fahari ya dunia hii lakini bado ukanisaliti.Penny I’m a powerful man in the country so I can do anything when I’m angry.Nakupa uhuru nieleze kitu chochote na kila unachokitaka nitakupatia lakini ubaki kuwa wangu peke yangu na usije ukanichanganya na mtu mwingine.” Akasema Dr Joshua
Penny akafuta machozi na kumtazama Dr Joshua kwa macho makali
“ Hukutakiwa kufanya vile.Hutakiwi kuwa na wivu na mimi,wewe ni mtu mwenye familia yako.You cant control me.You cant give me all that I want.You cant be there all the time when I need you.I’m a human Dr Joshua and I have needs” akasema penny kwa sauti ya juu
“ Penny mara ngapi nikwambie kwamba wewe ni kila kitu kwangu? Unataka niende katika luninga na kuutangazia ulimwengu kwamba ninakupenda? Niko tayari kufanya hivyo kama hiyo itakufanya uufungue moyo wako na kuniruhusu niingie ndani.Nipe nafasi ya kukuonyesha ni namna gani ninakupenda Penny.Forget that I’m married and I have a family.Not all marriages are real.Some are in papers. Kama ukinipa nafasi ndani ya moyo wako ,nitakuweka katika nafasi ya juu kuliko wanawake wote wa nchi hii.You’ll be the first lady.So why cant we skip the past and talk about our bright future? Akasema Dr Joshua Penny akamuangalia na kusema
“ Najaribu kukubaliana nawe lakini bado moyo wangu na maswali mengi ambayo yanahitaji majibu sahihi Dr Joshua.”
“ Just one question Penny.One question only” akasema Dr Joshua
“ Kwa nini kesi ile ya mauaji ya Edson iliniangukia mimi na ukakubali kuniona nikinusurika kuangamia wakati ukijua kabisa kwamba sikutenda kosa? Kwa nini hukufanya lolote kunisaidia kama kweli unanipenda?
“ Hayo ni maswali mawili Penny.Nitajibu swali moja tu” akasema Dr Joshua ,akanywa funda moja la mvinyo na kusema
“ I was angry” akasema na kunyamaza
“ I was angry for what you did to me and I wanted to destroy you.Nilitaka ufutike kabisa katika dunia hii,nilidhani kwamba ile ilikuwa ni njia muafaka ya kuweza kukusahau,but I was wrong.Penny naomba uelewe kwamba tayari umeniingia katika kila mshipa wa mwili wangu na siwezi kukutoa tena.Ninaomba utambue kwamba nilipata wakati mgumu sana kwa maamuzi yale na hilo ndilo jambo ambalo nitaendelea kulijutia hadi siku ninaingia kaburini.Tafadhali naomba utafute ndani ya moyo wako unisamehe na tuendelee na mapenzi yetu kama zamani.Nilifanya kosa kutaka kukupoteza mara ya kwanza safari hii sitaki tena kurudia kosa .Please lets not talk about the past .Lets not ruin our lovely night.Lets open new chapter in our book.” Akasema Dr Joshua kwa sauti ya kubembeleza,akamvuta Penny na kumkumbatia akambusu
“ Nimekwisha kusamehe Dr Joshua kwa sababu ninakupenda na ndiyo maana niko hapa ila tafadhali nakuomba usifanye tena jambo kama lile.Kama kuna tatizo kati yetu tafadhali naomba uniadhibu mimi na si watu wengine wasiokuwa na hatia.Please don’t hurt people that I love”
“ Siwezi kufanya hivyo tena kama utanihakikishia kwamba hautakuwa na mahusiano na mtu mwingine zaidi yangu. Niambie chochote kile nitakupatia Penny.I have power ,money and everything to make you live like a queen”
‘ Dr Joshua I’m still young and you are getting old.You have a family,you have a wife on bed,you have huge responsibilities and you cant be there all the time that I need you……………..” Penny hakumaliza sentensi yake Dr Joshua akamkatisha
“ I’ll be there ! Anytime you need me just call me and I’ll be there.Kwako sintakuwa na neno la hapana.Niambie chochote unachokitaka nitakutimizia” akasema Dr Joshua na kumfanya Penny atabasamu
“ This is the moment I’ve been waiting .Tayari ameingia mwenyewe katika nyavu na kilichobaki sasa ni kumvua tu.Ni wakati wangu sasa kumaliza kazi yangu” akawaza Penny
“ Dr Joshua kabla ya yote kuna jambo ambalo nataka nikuombe”akasema penny
“ Omba chochote Peniela.Kila kitu katika nchi hii kipo chini yangu” akasema Dr Joshua
“ Ninao watu wangu wawili ambao ni zaidi ya marafiki.Niko nao karibu sana watu hawa.Naomba kwa namna yoyote ile watu hawa wasije wakadhurika.Wana mchango mkubwa sana katika maisha yangu.Can you give me your word that you wont hurt them?” akasema Penny.Dr Joshua akatabasamu na kusema
“ I give you my word Penny.Who are they?
“ Wakili wangu Jason pamoja na Jaji Elibariki”
Dr Joshua akastuka kidogo baada ya kusikia jina la jaji Elibariki likitajwa
“ Usihofu Penny.Jaji Elibariki ni mwanangu.Amemuoa binti yangu. Ni kijana makini na mchapakazi na ndiyo maana nikamchagua kuwa jaji wa mahakama kuu.Nafahamu wewe na yeye ni marafiki na baada tu ya kumalizika kwa kesi mlikutana kwa chakula cha usiku.Nadhani ulikwenda kumshukuru kwa kukuachia huru” akasema Dr Joshua huku akicheka
“ Kwa hiyo umeweka watu wa kunifuatilia maisha yangu? Akauliza Penny
“ Ni kwa sababu ya usalama wako Penny.
“ Tafadhali naomba uwaondoe watu wako wasiendelee kunichunguza.I can defend myself.Siku nikigundua kwamba bado watu wako wanaendelea kunfuatilia it’ll be the end of us”
“ Ok Penny nitawaondoa kama ndivyo unavyotaka lakini ukumbuke kwamba wewe ni mke mtarajiwa wa rais kwa hiyo unahitaji ulinzi.Sema kingine unachokitaka” Penny akatabasamu na kusema
“ Kwa sasa kingine ninachokihitaji ni hiki” akasema na kulivuta taulo alilojifunga Dr Joshua na kumsukuma kitandani halafu akaanza tena kumfanyia utundu na baada ya dakika kadhaa wakaingia tena katika mzunguko mwingine.Ulikuwa ni usiku wa aina yake kwa Dr Joshua.
***********
Kengele ya mlangoni ililia kuashiria kwamba kuna mtu mlangoni.Mathew akainuka na kwenda kuufungua.
“ Anitha the devil ..!! akasema kwa furaha Mathew baada ya kuufungua mlango na kukutana na Anitha
“ Welcome my dear.Welcome home” akasema Mathew huku akikumbatiana na Anitha
“ Thank you so much Mathew.” Akasema Anitha
“ Ungenitaarifu muda ambao utatua ili nije nikupokee “ akasema Mathew
“ Usijali Mathew,hapa ni nyumbani na hauna haja ya kupoteza muda wa kufanya mambo mengine kwa kuja kunipokea.Npe habari kazi inaendeleaje? Akauliza huku akifungua friji na kutoa chupa ya mvinyo akajimiminia katika glasi.
“ Hautaki hata kupumzika Anitha? Pumzika kwanza halafu mambo ya kazi yatafuata baadae” akasema Mathew na kumfanya Anitha acheke kidogo
“ Mathew you know me,I work like a devil. Nimekuja kikazi kwa hiyo tufanye kazi na mambo mengine yatafuata baadae” akasema Anitha.Mathew akatasamu na kusema
“ Kazi tayari imeanza na mpaka sasa hakuna hatua kubwa iliyopigwa japo kuna mwangaza kidogo tayari nimeupata” akasema Mathew.Anitha akageuza kichwa na kumtazama Mathew akasema
“ Nilipata kazi ya pesa nyingi nchini Brazil ambayo nilitakiwa nikaifanye wiki hii lakini nimelazimika kuweka pembeni kwanza ile kazi na kuja kuimaliza kwanza kazi uliyoniitia. Nipe taarifa za kina kuhusiana na kazi hii” akasema Anitha huku akiifungua mizigo yake na kutoa zana zake za kazi
“ Ahsante sana Anitha kwa kuahirisha mambo yako mengine na kuja kuungana nami.Hata mimi pia nimelazimika ksimamisha baadhi ya shughuli zangu kwa ajili ya shughuli hii. Si kazi yenye malipo makubwa lakini ni muhimu sana kwa rafiki zangu” akasema Mathew
“ Kuna kijana mmoja aitwaye Edson,ambaye alikuwa mfanyakzi wa kitengo cha mawasiliano ikulu,aliuawa na watu wasiofahamika na kesi hiyo kumuangukia msichana mmoja aitwaye Peniela . Jaji Elibariki ambaye alikuwa akiisikiliza kesi ile aligundua kwamba msichana Yule aliyekuwa akituhumiwa hakutenda kosa hivyo akalazimika kumuachia huru.Baada ya kesi kumalizika alishawishika kufanya uchunguzi wa kina kuhusiana na kesi ile kutokana na sintofahamu kadhaa alizozigundua wakati wa usikilizwaji wa kesi.Aliungana na wakili Jason aliyekuwa anamtetea mtuhumiwa na kwa pamoja wakaamua kunipa kazi hii kutokana na kwamba wao hawana taaluma ya uchunguzi.Kwa hiyo naomba ufahamu kwamba tunaifanya kazi hii kuitafuta haki na vile vile kuwasaidia rafiki zetu” akasema Mathew
“ Kesi hii inafanana na ile ya Justine Abangiza wa Rwanda” akasema Anitha huku akiunganisha vifaa vyake
“ Yah ! zinashabihiana sana ingawa hii ya Edson ina utofauti kidogo” akasema Mathew
“ Nimeongea na wazazi wake jioni ya leo .Nilitaka tu kufahamu mtoto wao alikuwa ni mtu wa namna gani.Kabla ya hapo mchana wa leo nilikwenda nyumbani kwa Peniela,msichana aliyetuhumiwa kumuua Edson, na kutega kamera mbili ,niliporudi nimekutana na picha hizi” akasema Mathew na kumuonyesha Anitha zile picha za wale watu walionaswa katika kamera nyumbani kwa Penny
“ They look so professional “ akasema Anitha
“ Yah ! Wanaonekana wazoefu sana .Ninachojiuliza ni kwa nini wametega kamera mlangoni kwa Penny?
“ Jibu ni jepesi Mathew,Wanataka kuangalia kila kinachoendelea nyumbani kwa Penny.Cha kujiuliza ni kwa nini wanataka kutazama kila kinachoendelea nyumbani kwa Penny?Kwa nini Peniela anachunguzwa? Au watu hawa yawezekana wakawa ni walinzi binafsi wa Peniela? Akauliza Anitha
“ Sina hakika kama watu wale ni walinzi wa Peniela kutokana na namna walivyoingia.Wanaonekana wazi kufahamu kwamba muda ule Peniela hakuwepo nyumbami ndiyo maana waliingia kwa kunyata na kuweka ile kamera nadhani kwa lengo la kutaka kufahamu mienendo ya Penny.Tunachotakiwa kufahamu watu hawa ni akina nani na nini lengo lao la kumchunguza Penny.Tayari tuna sehemu nzuri sana ya kuanzia uchunguzi wetu.Sehemu nyingine ya kufanyia uchunguzi ni katika laini ya simu ya Edson. Wauaji waliondoka na simu na pamoja na kompyuta zake zote.Inaonekana wazi kwamba kuna kitu kilichokuwa kinafichwa na ndiyo maana wauaji wale hawakuwa na shida na pesa na wakaondoka na vitu hivyo tu.Wakati wa kuhamisha vifaa vyake,ilipatikana laini ya simu ikiwa imefichwa katika chungu cha maua.Sielewi ni kwa nini aliificha laini hii ya simu lakini nina imani hakutaka ionekane kwa sababu maalum.Inaweza ikawa na msaada kwetu.Tunatakiwa tuichunguze laini hii pia” akasema Mathew.Anitha hakujibu kitu aliendelea na kazi yake ya kuunganisha mitambo yake. Nusu saa baadae alimaliza kuunganisha mitambo yake akaiwasha na kujaribu
“ Everything is in position.We can start our job now” akasema Anitha

SEHEMU YA 17
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Tunachotakiwa kufahamu watu hawa ni akina nani na nini lengo lao la kumchunguza Penny.Tayari tuna sehemu nzuri sana ya kuanzia uchunguzi wetu.Sehemu nyingine ya kufanyia uchunguzi ni katika laini ya simu ya Edson. Wauaji waliondoka na simu na pamoja na kompyuta zake zote.Inaonekana wazi kwamba kuna kitu kilichokuwa kinafichwa na ndiyo maana wauaji wale hawakuwa na shida na pesa na wakaondoka na vitu hivyo tu.Wakati wa kuhamisha vifaa vyake,ilipatikana laini ya simu ikiwa imefichwa katika chungu cha maua.Sielewi ni kwa nini aliificha laini hii ya simu lakini nina imani hakutaka ionekane kwa sababu maalum.Inaweza ikawa na msaada kwetu.Tunatakiwa tuichunguze laini hii pia” akasema Mathew.Anitha hakujibu kitu aliendelea na kazi yake ya kuunganisha mitambo yake. Nusu saa baadae alimaliza kuunganisha mitambo yake akaiwasha na kujaribu
“ Everything is in position.We can start our job now” akasema Anitha
ENDELEA…………………………..
“ Kazi ya kwanza ambayo tunaweza kuifanya usiku wa leo ni kuichunguza laini hii ya simu ili tufahamu Edson alikuwa akiwasiliana na akina nani kwa siri.Tukiwafahamu watu ambao aliwasiliana nao kwa siri kuna jambo tunaweza tukalipata toka kwao.Nina hakika lazima kuna sababu iliyomfanya Edson akaificha laini hii isionekane na mtu yeyote” akasema Mathew na kumpa Anitha ile laini ya simu akaipachika katika kifaa fulani kidogo mithili ya mkebe na kuanza kuibonyeza kompyuta yake.Baada ya sekunde kadhaa Anitha akaguna
“ Vipi mbona unaguna Anitha? akauliza Mathew
“ Laini hii ya simu imewekewa uzio.” Akasema Anitha
“ Una maana gani unaposema uzio?
“ Nina maana kwamba mtumiaji aliiwekea program maalum ambayo inaiwezesha laini hii ya simu kutumika katika simu yake tu .Inaonekana huyu jamaa alikuwa ana ufahamu mkubwa sana wa kompyuta”
“ Unaweza kuiondoa hiyo program? Akauliza Mathew
“ Ndiyo.Ninaweza kuiondoa.Hivi ni vitu vidogo sana kwangu” akasema Anitha huku akiendelea kucheza na kompyuta yake.Baada ya dakika saba akaegemea kiti na kuvuta pumzi ndefu
“ Tayari”
“ Congraturations” akasema Mathew lakini mara Anitha akaguna tena
“ This is strange !..Anitha akashangaa
“ Nini Anitha?
“ Inaonekana Edson alitumia laini hii ya simu kuwasiliana na watu wawili pekee.”
“ watu wawili ?! Mathew naye akashangaa
“ Ndiyo.Ameitumia kwa watu wawili tu”
“ Unaweza ukatafuta ni akina nani hao?
Anitha akaendelea kubonyeza kompyuta yake na baada ya dakika nne akasema
“ Kwa mujibu wa taarifa toka kampuni ya simu ya Tanphone namba hizo ni za Hellen Francis Kobe na nyingine ni ya Brigita samini.Inaonyesha Edson na Brigita wamekuwa wakiwasiliana mara kwa mara na hata siku moja kabla ya kifo chake Edson aliongea na Brigita kupitia laini hii.” Akasema Anitha
“ Hellen francis Kobe ni mama yake mzazi Edson na alinieleza kwamba kuna siku mwanae alimpigia simu kwa kutumia namba ngeni nadhani ni hii.Huyu Brigita simfahamu ni nani.Inawezekana alikuwa ni mtu muhimu sana kwa Edson na ndiyo maana akawa akitumia laini ya pekee kuwasiliana naye.” Akasema Mathew na kuziandika namba zile za Brigita katika simu yake akajaribu kupiga lakini hazikuwa zikipatikana.
“ Inawezekana mawasiliano ya watu hawa wawili yalikuwa ni ya siri mno.Inawezekana hata huyu Brigita hii akawa na laini ya ya siri ambayo huitumia kuwasiliana na Edson” akasema Mathew na kuzitafuta namba za simu za mzee Robinson Kobe na kumpigia
“ Hallo Mathew” akasema mzee Roinson baada ya kupokea simu
“ Samahani mzee wangu kwa kukupigia simu mida hii” akasema Mathew
“ Bila samahani Mathew.Kuna kitu chochote ninachoweza kukusaidia?
“ Ndiyo mzee.Ninataka kujua kama unamfahamu mtu anayeitwa Brigita Samini”
Kimya cha sekunde kadhaa kikapita halafu mzee Robinson akasema
“ Ninamfahamu Brigita.Edson aliwahi kunitambulisha kwake kwamba ni marafiki wakubwa.Brigita anafanya kazi katika hoteli ya kitalii ya Potina palace.”
“ Ok ahsante sana mzee” akasema Mathew na kukata simu
“ Brigita na Edson ni marafiki wakubwa kwa mujibu wa mzee Robinson.” Mathew akamwambia Anitha
“ Kama walikuwa na urafiki mkubwa kwa nini basi wawasiliane kwa siri? Akauliza Anitha
“ Hicho ndicho tunachotakiwa kukifahamu. Haiingii akilini kama watu ni marafiki wakubwa halafu wawasiliane kwa siri.Lazima kuna sababu iliyowafanya wawe na mawasiliano ya siri ” akasema Mathew na kuchukua kitabu chenye namba za simu za makampuni mbali mbali akaitafuta Potina palace hoteli anayofanya kazi Brigita.Akaipata na kuchukua namba zao za simu akapiga.
“ Karibu Potina palace nikusaidie nini? Ikasema sauti nzuri ya mwanadada baada ya kupokea simu
“ Namtafuta dada mmoja anaitwa Bigita Samini ni mfanyakazi wa hapo hotelini kwenu” akasema Mathew
“ Wewe ni ndugu yake?
“ Hapana mimi ni rafiki yake “
“ Samahani ndugu yangu Brigita hatunaye tena hapa hotelini.Alikwisha fariki dunia.”
“ Amefariki dunia?
“ Ndiyo alifariki dunia “
“ Alifariki lini na nini kilimuua?
“ Alilipukiwa na gesi na kufariki yeye na familia yake yote yapata mwaka sasa” akasema Yule dada na kumtajia Mathew tarehe ambayo Brigita alifariki dunia.Mathew akashukuru na kukata simu.
“ Vipi wanasemaje? Akauliza Anitha
“ Mambo yanazidi kuibuka.Brigita alifariki dunia wiki moja tu baada ya Edson kufariki dunia.Alilipukiwa na gesi na wakafariki yeye na familia yake yote ” akasema Mathew na kimya kikapita
“ Walikuwa wakiwasiliana kwa siri na hata vifo vyao vimetokea kwa kufuatana.Mathew kuna kitu hapa si bure.Kama walikuwa ni marafiki kuna jambo lazima watakuwa wakilifahamu kwa pamoja au wakilificha na ndiyo maana hata mawasiliano yao yalikuwa ya siri kubwa na hawakutaka mtu mwingine yeyote Yule afahamu kama walikuwa wakiwasiliana.Siri hiyo waliyokuwa wakiificha ndiyo iliyowagharimu maisha yao.” Akasema Anitha
“ Anitha inatosha kwa leo.Tupumzike na kesho tuanze kazi rasmi.Tutaanza kazi kwa kutafuta taarifa za Brigita Samini .Anaonekana ni mtu muhimu sana katika suala hili” akasema Mathew.Anitha akamtazama na kutabasamu halafu akazima kompyuta zake
“ Uko sahihi Mathew.Leo imekuwa ni siku ndefu sana.Tupumzike ili kesho tuanze kazi “ akasema Anitha
TUKUTANE SEHEMU IJAYO…SEASON 1
SEHEMU YA 18
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ Walikuwa wakiwasiliana kwa siri na hata vifo vyao vimetokea kwa kufuatana.Mathew kuna kitu hapa si bure.Kama walikuwa ni marafiki kuna jambo lazima watakuwa wakilifahamu kwa pamoja au wakilificha na ndiyo maana hata mawasiliano yao yalikuwa ya siri kubwa na hawakutaka mtu mwingine yeyote Yule afahamu kama walikuwa wakiwasiliana.Siri hiyo waliyokuwa wakiificha ndiyo iliyowagharimu maisha yao.” Akasema Anitha
“ Anitha inatosha kwa leo.Tupumzike na kesho tuanze kazi rasmi.Tutaanza kazi kwa kutafuta taarifa za Brigita Samini .Anaonekana ni mtu muhimu sana katika suala hili” akasema Mathew.Anitha akamtazama na kutabasamu halafu akazima kompyuta zake
“ Uko sahihi Mathew.Leo imekuwa ni siku ndefu sana.Tupumzike ili kesho tuanze kazi “ akasema Anitha
ENDELEA…………………………..
Kumekucha Dar es salaam,saa tatu za asubuhi Iliwakuta Mathew na Anitha nje ya hoteli ya kitalii ya Potina Palace.Waliegesha gari na kushuka wakaingia hotelini na moja kwa moja wakaelekea mapokezi ambako walimkuta mwanadada mmoja mrembo wakajitambulisha kama rafiki wa Brigita Samini aliyekuwa akifanya kazi pale hotelini.Yule mwanadada wa mapokezi akashangaa kidogo na kuuliza
“ Hamkuwa na mawasiliano naye au ndugu zake?
“ Sisi tunaishi Marekani na kwa muda msrefu kidogo hatukuwa tumewasiliana naye.Mara ya mwisho tulipowasiliana naye alituelekeza kwamba anafanya kazi hapa.” Akasema Mathew
“ Poleni sana ndugu zangu.Brigita hatuko naye tena,alifariki dunia yapata mwaka mmoja sasa umepita” akasema yule dada ambaye kitambulisho cha kazi alichokivaa kilionyesha anaita Stella manana .Mathew na Anitha wakaonyesha mstuko ili kumfanya Yule dada asiwe na wasi wasi wowote kuhusu wao.
“ Nini ilikuwa sababu ya kifo chake? Akauliza Anitha
“ Mtungi wa gesi ulilipuka na kusababisha nyumba yao iteketee kwa moto.Hakuna hata mtu mmoja aliyetoka hai.Ilikuwa ni ajali mbaya sana.Brigita alikuwa ni meneja wetu na mtu mwenye roho nzuri sana na kila mtu hapa alimpenda “
Kikapita kimya cha sekunde kadhaa Mathew akauliza
“ Kuna mtu yeyote ambaye alikuwa ni mtu wake wa karibu sana ili aweze kutuelekeza kwa ndugu zake tukawape pole? Akauliza Mathew
“ Brigita alikuwa na marafiki wengi na kila mtu alikuwa ni rafiki yake lakini kuna mmoja ambaye alikuwa ni rafiki yake mkubwa anaitwa Subira.Kwa sasa hayupo hapa hotelini anasomea shahada ya hoteli pale Ikandala University.Kama mnahitaji taarifa za kina kuhusiana na Brigita mtafuteni huyo Subira kwani ni yeye anayewafahamu hadi ndugu zake “ akasema Yule dada na kuwapatia namba za simu za Subira wakaagana Mathew na Anitha wakarejea katika gari lao.
“Mpigie simu Subira tufahamu yuko wapi” akasema Mathew.Anitha akaziandika zile namba katika simu yake na kupiga.Simu ikaita na kukatika,akapiga tena ikaita lakini haikupokelewa
“ Simu yake inaita tu lakini haipokelewi” akasema Anitha
“ Jaribu tena kumpigia.Isipopokelewa tutamfuata pale pale chuoni kwao” akasema Mathew ,Anitha akapiga tena na safari hi ikapokelewa
“ Hallow !..Ikasema sauti ya mwanadada upande wa pili
“ Hallow naongea na nani? Akasema Anitha
“ Unaongea na Subira Abdul.Wewe ni nani mwenzangu?
“ Ninaitwa Anitha”
“ Nikusaidie nini Anitha? Akauliza Subira ambaye alikuwa na sauti ya upole
“ Subira ninahitaji kukuona.Nina maongezi nawe kidogo” akasema Anitha
“ Una maongezi na mimi? Subira akashangaa
“ Ndiyo Subira.Nahitaji sana kukuona”
“ Ni maongezi kuhusu nini? Halafu mbona sikufahamu?
“ Usihofu Subira.Hata mimi sikufahamu nimepewa namba zako za simu pale Potina Palace ulipokuwa ukifanyakazi kabla ya kuanza kusoma.”
“ Ok Unataka tuongee jambo gani?
“ Mimi ni rafiki wa siku nyingi wa Brigita Samini ambaye nimeelezwa kwamba wewe ulikuwa na ukaribu naye mkubwa .Ninaishi Marekani kwa sasa na nimekuja kwa mapumziko mafupi.Nimeenda kumtembelea Brigita mahala nilikomuacha akifanya kazi kipindi cha kama mwaka mmoja uliopita nikaambiwa kwamba alifariki dunia katika ajali ya moto.Nimestuka sana .Ninataka kufahamu mengi kuhusiana na kifo hicho na hata kuwafahamu ndugu zake ili nikatoe pole.Nimeelekezwa kwako kwamba unaweza ukanisaidia kwa hilo Subira” akasema Anitha
“ Kwa sasa uko wapi? Subira akauliza
“ Kwa sasa ninaondoka hapa Potina Palace.wewe uko wapi?
“ Mimi niko chuoni hapa Ikandala University.Ninamalizia kipindi cha mwisho .Unaweza ukaja kunisubiri hapa chuoni nimalize kipindi?
“ Usijali Subira ninakuja” akasema Anitha na kukata simu
“ Yuko chuoni anamalizia kipindi,anasema tumfuate tukamsubiri” Anitha akamwambia Mathew
Wakiwa njiani, kuelekea chuoni,Mathew akawasiliana na Jason kutaka kujua kama Penny amekwisha rejea lakini mpaka muda huo Jason hakuwa na taarifa zozote za kumuhusu Penny
“ Penny atakuwa amekwenda wapi? Mpaka leo hajaonekana na hajulikani yuko wapi” akasema Mathew
“ Unahisi anaweza kuwa amepatwa na tatizo? Akauliza Anitha
“ Sina hakika sana lakini hata kama hajapatwa na tatizo bado hayuko salama.Bado nawafikiria watu wale walioingia ndani ya nyumba yake jana na kuweka kamera za siri ni akina nani na wana lengo gani kwa Penny.Nashawishika kutaka kumfahamu vizuri zaidi Penny.” Akasema Mathew
“ Have you met her? Akauliza Anitha huku akiendelea kucheza na kompyuta yake
“ No I haven’t” akajibu Mathew
Waliendelea na safari hadi walipofika Ikandala University,Anitha akamtumia Ujumbe Subira kumfahamisha kwamba tayari wamekwisha fika wako nje wanamsubiri.Baada ya dakika ishirini Subira akatoka.Hakuwa akimfahamu Anitha hivyo ikamlazimu kumpigia simu ,Anitha akamuelekeza mahala walipo akawafuata
“ Habari yako Subira” akasema Anitha.Subira alionyesha hofu kidogo alipogundua kwamba Anitha hakuwa peke yake bali alikuwa na Mathew
“ Habari yangu nzuri.habari zenu?
“ Habari zetu nzuri.Pole na masomo”
“ Ahsante” akajibu Subira
“ Subira huyu hapa ni mwenzangu anaitwa Mathew kwa hiyo naomba usiwe na hofu.” Anitha akafanya utambulisho kwani alimuona Subira akiingiwa na uoga.
“ Subira hatutaki kuchukua muda wako mwingi kwani najua una shughuli nyingi za kufanya.Tunaweza kupata sehemu hapa karibu tukakaa na kuongea japo kwa dakika chache? Akauliza Anitha
“ Kuna hoteli pale karibu tunaweza kwenda kukaa tukaongea” akajibu Subira halafu wakaongozana kuelekea katika hoteli iliyokuwa kandoni mwa chuo.
“ Subira kama tulivyoongea simuni,mimi ni rafiki wa siku nyingi wa Brigita.Kwa sasa ninaishi Marekani na nimerudi nchini kwa mapumziko mafupi.Ni muda umepita sijawasiliana naye na mara ya mwisho kuwasiliana naye alinielekeza mahala anapofanyia kazi nikamwambia kwamba nikija Tanzania nitamtembelea.Nimefika kumtembelea mahala alikonielekeza anafanya kazi nikakutana na taarifa hizi za kustusha za kifo chake.Nimeumia sana.Hebu nieleze japo kwa undani kidogo nini kilitokea na kusababisha kifo chake? Akauliza Anitha.
Subira akavuta pumzi ndefu na kusema
“ Brigita alikuwa ni rafiki yangu mkubwa na tulikuwa tunaelewana mno.Usiku wa siku alipofariki tulipanga twende taarabu mashauzi Classic lakini baadae alibadili maamuzi na kuniambia kwamba hangekwenda tena Mashauzi kwani alipigiwa simu na babu kwamba wanatakiwa waonane jioni ya siku ile.Safari yetu ikawa imeishia hapo,hatukutoka tena hadi nilipopata taarifa za kifo chake asubuhi.Kwa kweli hata mimi niliumia mno na hadi leo hi bado ninaendelea kuumia.Nilimpenda sana Brigita.Kwa mujibu wa uchunguzi uliofanywa inasemekana kwamba mtungi wa gesi ulilipuka na kusababisha maafa yale” akasema Subira
“ Pole sana Subira” akasema Anitha
“ Nimekwisha poa” akajibu subira
“ Umesema kwamba mlipanga muende mashauzi Classic lakini mkaahirisha aliposema kwamba alipigiwa simu akaonane na babu.Huyu babu ni nani?
Subira akatabasamu kidogo na kusema
“ Brigita alikuwa na mahusiano na mzee mmoja hivi ambaye ndiye aliyemjengea nyumba,akamnunulia gari na ndiye aliyekuwa akimuhudumia kwa kila kitu.Mzee Matiku alifariki dunia wiki mbili tu baada ya Brigita kufariki kwa kujipiga risasi ya kichwa.Inasemekana kifo cha Brigita kilimuumiza sana na ndiyo maana akaamua kujimaliza kwa risasi. ”
“ Dah ! akasema Anitha
“ Nakumbuka Brigita aliwahi kuwa na mahusiano na kijana mmoja hivi anaitwa Edson.Aliwahi kunitumia picha wakiwa naye.Gosh he was very handsome,je waliachana hadi akaamua kuingia katika mahusiano na huyo mzee? Akauliza Anitha
“ Edson ninamfahamu lakini naye alikwisha fariki dunia.Aliuliwa na mpenzi wake.Ninachokifahamu mimi,Brigita na Edson walikuwa wanakutana kwa siri.Hakuwa akimpenda mzee Matiku na alikuwa naye kwa ajili ya pesa zake tu lakini moyo wake ulikuwa kwa Edson.Mzee Matiku alikuwa na wivu uliopitiliza na aliwahi kumwambia Brigita kwamba siku akimkuta na mwanaume mwingine basi huo ungekuwa ni mwisho wake.Brigita alimuogopa sana mzee Yule hivyo akawa akiwasiliana na Edson kwa siri.Mzee Edson alikuwa akimfuatilia sana hadi alimuwekea kifaa maalum katika simu yake cha kuchunguza watu aliokuwa akiwasiliana nao.Hakutaka kabisa amuone na mwanaume yeyote zaidi yake.Brigita alianza kuchoshwa na mahusiano yake na Yule mzee na kila siku alikuwa akiniambia kwamba siku moja lazima atakuja kumkimbia .Aliniambia kwamba kuna biashara wanataka kuifanya na Edson na endapo ikifanikiwa basi watapata pesa nyingi na kisha atamkimbia mzee yule na kuhama kabisa nchi.Hakuwahi kuniambia ni biashara gani walitegemea kuifanya na Edson.Siku moja aliniambia kwamba kuna kitu amekichukua toka kwa mzee Matiku ambacho endapo angegundua basi kingemletea shida sana.Hakuniambia ni kitu gani hadi alipofariki.” Akasema Subira
“ Huyo mzee Matiku alikuwa anafanya kazi gani? Alikuwa na familia?
“ Mzee Matiku ni mfanyabiashara,ndiye mwenye ile hoteli niliyokuwa nikifanya kazi na ndiyo maana Brigita alikuwa na kazi nzuri sana pale.Watu wanasema kwamba ni mwanajeshi mstaafu.Wanasema kwamba aliwahi kuwa mlinzi wa rais miaka ya nyuma sana.Kwa upande wa familia mzee Matiku hakuwa na familia” akasema Subira.
“ Subira nashukuru sana kwa kunipa mwanga kuhusiana na kifo cha rafiki yangu Brigita.Kwa sasa kuna mahala ninatakiwa kwenda ila nitakutafuta mwishoni mwa wiki tukae tuongee na unieleze mambo mengi kuhusiana na Brigita na pia unitambulishe kwa ndugu zake unaowafahamu ili niweze kuwapa pole.Ahsante sana kwa muda wako na tutaonana tena” akasema Anitha huku akifungua pochi yake na kumpatia Subira kiasi cha dola hamsini za Marekani halafu wakasimama na kuondoka
“mambo mapya yanazidi kuibuka kila siku.Kwa sasa tuna mtu mwingine ameongezeka katika uchunguzi wetu,babu Matiku.” Akasema Mathew wakiwa garini wakiondoka maeneo ya chuo
“ Brigita alikuwa na mahusiano na mzee Matiku na wakati huo huo akawa na mahusiano ya siri na Edson.Walikuwa wakiwasiliana kwa siri ili mzee Yule asigundue na ndiyo maana laini ile ya simu ya Edson iliwekewa uzio ili mtu mwingine asiweze kugundua walichokuwa wakikiongea.Kwa mujibu wa Subira siku chache kabla ya kifo chake Brigita alimweleza kwamba kuna kitu alikichukua toka kwa mzee Matiku je ni kitu gani hicho? Ni biashara gani aliyokuwa akiifanya na Edson ambayo ingewapatia pesa nyingi kiasi cha kumfanya Brigita afikirie hatan kukimbia na kuhama nchi? Akauliza Mathew
“ Majibu ya maswali haya yanakuwa magumu kupatikana kwa sababu wahusika wote ambao wangeweza kutupatia majibu wamekwisha fariki.Tumerudi katika sifuri .Lakini kuna muunganiko wa kifo cha Edson,Brigita na mzee Matiku.Sababu ya vifo vyao ni moja.Ninahisi hicho kitu Brigita alichokichukua toka kwa mzee Matiku alimshirikisha pia Edson na inawezekana ndiyo iliyosababisha vifo vyao.Je ni kitu gani hicho? Ni biashara gani walitaka kuifanya? Mzee matiku ni nani? Nadhani ili tupate mwangaza tunatakiwa tumfahamu pia huyu mzee ni nani ,vyanzo vyake vya mapato n.k.Yawezekana akawa ni mtu aliyekuwa akijishughulisha na biashara ya madawa ya kulevya..” akasema Mathew lakini akastuliwa na Anitha
“Mathew…!!” Anitha akaita
“ Kamera kipepeo nyumbani kwa Penny imetoa mlio.Kuna watu wanaingia nyumbani kwa Penny” akasema Anitha.Mathew akasogeza gari pembeni na kusimama akawatazama watu wale waliokuwa wakiinga kwa Penny kupitia kompyuta ya Anitha
“ Ni sura zile zile za jana.Who are these people? Wanatafuta nini kwa penny?
“ We need to find out” akasema Mathew huku akiwashuhudia watu wale wakiufungua mlango wa Penny na kuingia ndani
“ Twende nyumbani kwa Penny.Leo lazima tuwafahamu” akasema Mathew na kuwasha gari wakaelekea nyumbani kwa Penny
TUKUTANE SEHEMU IJAYO…SEASON 1
SEHEMU YA 19
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ Majibu ya maswali haya yanakuwa magumu kupatikana kwa sababu wahusika wote ambao wangeweza kutupatia majibu wamekwisha fariki.Tumerudi katika sifuri .Lakini kuna muunganiko wa kifo cha Edson,Brigita na mzee Matiku.Sababu ya vifo vyao ni moja.Ninahisi hicho kitu Brigita alichokichukua toka kwa mzee Matiku alimshirikisha pia Edson na inawezekana ndiyo iliyosababisha vifo vyao.Je ni kitu gani hicho? Ni biashara gani walitaka kuifanya? Mzee matiku ni nani? Nadhani ili tupate mwangaza tunatakiwa tumfahamu pia huyu mzee ni nani ,vyanzo vyake vya mapato n.k.Yawezekana akawa ni mtu aliyekuwa akijishughulisha na biashara ya madawa ya kulevya..” akasema Mathew lakini akastuliwa na Anitha
“Mathew…!!” Anitha akaita
“ Kamera kipepeo nyumbani kwa Penny imetoa mlio.Kuna watu wanaingia nyumbani kwa Penny” akasema Anitha.Mathew akasogeza gari pembeni na kusimama akawatazama watu wale waliokuwa wakiinga kwa Penny kupitia kompyuta ya Anitha
“ Ni sura zile zile za jana.Who are these people? Wanatafuta nini kwa penny?
“ We need to find out” akasema Mathew huku akiwashuhudia watu wale wakiufungua mlango wa Penny na kuingia ndani
“ Twende nyumbani kwa Penny.Leo lazima tuwafahamu” akasema Mathew na kuwasha gari wakaelekea nyumbani kwa Penny
ENDELEA…………………….
“ Wanafungua mlango wa sebuleni ,wanaingia ndani” akasema Anitha aliyekuwa akiwatazama wale jamaa kupitia kompyuta iliyounganishwa na kamera zilizoko nyumbani kwa Peniela
“ Kwa bahati mbaya hakuna kamera yoyote niliyoweka ndani ya nyumba ya Penny kwa hiyo hatuwezi kujua wanakwenda kutafuta kitu gani mle ndani lakini leo lazima tupate majibu watu hawa ni akina nani na wanatafuta nini kwa Penny” akasema Mathew ambaye alikuwa makini sana katika usukani
Waliwasili katika mtaa anaoishi Penny wakasimamisha gari nyumba ya tatu toka nyumba ya Penny.
“ We’re here.Nyumba ya Penny ni ile yenye bati jekundu.Ngoja tuendelee kuwasubiri wale jamaa watoke” Mathew akamuonyesha Anitha nyumba ya Penny
“ Wow ! Nyumba nzuri sana.Anafanya kazi gani Penny? Akauliza Anitha
“ Penny ni mfanya biashara.Ana maduka makubwa ya urembo na mavazi” akajibu Mathew
Waliendelea kukaa ndani ya gari wakiikodolea macho kompyuta na mara mlango wa mbele wa nyumba ya Penny ukafunguliwa
“ Wanatoka” akasema Anitha
“ Ok Get ready” akasema Mathew huku akiwasha gari
Wale jamaa walitoka wakafunga geti na kuingia katika gari lao wakaondoka.Mathew na Anitha wakawafuata
Toka nyumbani kwa Penny ,walielekea hadi katika duka moja la kuuza vyakula mmoja wao akashuka na kuingia ndani ya duka lile na baada ya muda mfupi akatoka akiwa na mfuko mkononi ,wakaendelea na safari yao bila kujua kama walikuwa wakifuatiliwa na akina Mathew
Saa sita na dakika nane wakawasili Miseko hospital,moja kati ya hospitali kubwa nchini.
“ Wamefuata nini hapa hospitali? Akauliza Mathew
“ Lazima kuna kitu wamekifuata hapa.Tuendelee kuwafuatilia.Ninaingia katika mfumo wa kompyuta wa hapa hospitali ili niweze kuwafuatilia kupitia kamera za ulinzi zilizoko hapa hospitali “ akasema Anitha
Wale jamaa wakashuka garini na kuangaza huku na huko halafu wakaanza kutembea kwa kasi kuelekea kusini mwa hospitali kuliko na wodi za kulipia na zile wa watu maarufu
“ Wanaonekana kuelekea sehemu ziliko wodi za watu maarufu.Anitha wewe utabaki ndani ya gari mimi nitawafuatilia nione wanakwenda kufanya nini kule katika wodi.Endelea kuwafuatilia kupitia kamera “ akasema Mathew huku akiweka sikioni kifaa cha mawasiliano kati yake na Anitha.Akakijaribu na kuona kinafanya kazi ,akashuka garini
“ I’m in now.I can access every thing.Ninawaona wale jamaa kwa kupitia kamera 4g ambayo imeelekezwa kusini” Anitha akamtaarifu Mathew aliyekuwa akitembea kwa kasi kuwafuata wale jamaa ambao hawakuwa na wazo kwamba wanafuatiliwa
“ Good Job Anitha,keep an eye on them” akasema Mathew. Ukubwa wa hospitali hii ulichangia kuwepo kwa idadi kubwa ya watu.Karibu magonjwa yote yalikuwa yakitibiwa hapa hivyo hospitali hii ilikuwa ikipokea mamia ya wagonjwa kila siku toka katika sehemu mbali mbali za nchi na hata nchi za jirani
“ Mathew nimebadilisha kamera na sasa natumia kamera 6 C” Anitha akamtaarifu Mathew
“ Ok Anitha.Endelea kuwafuatilia.Hata mimi bado sijawapoteza.Niko nao sambamba” akasema Mathew
Wale jamaa walinyooka na kuingia katika jengo lililokuwa na kibao VIP Private 2.
“ Wanaingia VIP Private 2” Mathew akamwambia Anitha
“ Ok nimekwisha waona.Itabidi ufanye haraka ili usiwapoteze kwa sababu mle ndani ninaiona kamera moja tu inayofanya kazi .Kamera nyingine zote inaonekana hazifanyi kazi.” akasema Anitha.Mathew akaongeza mwendo na kuacha umbali mfupi baina yake na wale jamaa.Watu wale hawakutaka kutumia lifti ,wakapanda ngazi kwa miguu hadi ghorofa ya nne ambayo ilionekana kuwa kimya sana.Wale jamaa wakasimama nje ya mlango mmoja wakagonga na baada ya sekunde kadhaa mlango ukafunguliwa wakaingia ndani. Mathew aliyekuwa akitembea kwa uangalifu mkubwa ili wale jamaa wasije wakastuka kwamba anawafuatilia akatazama pande zote hakuona mtu,akaukaribia mlango ule na kusoma namba zilizobandikwa juu.
“ Anitha wameingia chumba namba PV2 – 78.Angalia katika orodha ya wagonjwa tufahamu ni nani aliyelazwa katika chumba hiki” akasema Mathew.Baada ya kama dakika moja Anitha akasema
“Katika chumba hicho amelazwa mgonjwa mmoja anaitwa John Mwaulaya Albert,anasumbuliwa na tatizo la kupoteza fahamu mara kwa mara”
Mathew akastuka sana aliposikia jina lile la John Mwaulaya Albert
“ Anitha umesema John Mwaulaya Albert? akauliza Mathew
“ Ndiyo.Do you know him? Akauliza Anitha.Mathew hakujibu kitu .Alionekana wazi kupatwa na mstuko
“ Mathew say something.Do you know him? Akauliza tena Anitha
“ Subiri kidogo Anitha” akasema Mathew halafu akaukaribia ule mlango na kujaribu kutega sikio ili asikie kinachoongelewa ndani lakini hakusikia chochote.Alionekana kuchanganyikiwa ghafla
********
Gari mbili nyeusi ziliwasili katika eneo la kuegeshea magari katika uwanja wa kimataifa wa ndege wa Kilimanjaro .Watu wanne waliovalia suti nyeusi wakashuka wawili toka katika kila gari.Mlango wa kati wa gari lililotangulia ukafunguliwa na mwanadada mmoja mwenye uzuri wa kimalaika akashuka.Alikuwa amevalia koti kubwa la kujikinga na baridi.Toka katika gari la pili,mabegi matatu yakashushwa na kuanza kukokotwa kuelekea ndani ya uwanja wa ndege kulikokuwa na ndege maalum iliyoandaliwa kwa ajili ya mwanadada huyu mwenye uzuri usio na kifani.Baada ya hatua kama tano hivi ,simu ya mmoja wa wale vijana ikaita akaipokea na kisha akampatia Yule mwanadada waliyekuwa wameongozna naye
“ Madam Penny mheshimiwa rais anataka kuongea nawe.” Akasema Yule jamaa .Penny akaichukua ile simu na kuiweka sikioni
“ hallo” akaita
“ Hallo my angel.Tayari umeshafika uwanja wa ndege? I’ve missed you already” akasema Dr Joshua rais wa jamhuri ya mungano wa Tanzania
“ I’ve missed you too Dr Joshua,hivi sasa ndio tumewasili uwanjani tunaelekea ndegeni”
“ Penny ,hakuna sababu ya msingi iliyonifanya nikupigie simu .I just…I ..Just want to talk to you,to hear your voice and tell you how much I do miss you.Peniela thank you so much for everything.” Akasema Dr Joshua
Peny akatabasamu na kusema
“ Thank you too Dr Joshua for everything.You know how to treat a woman.You made me so happy.” Akasema Penny
“ Nafurahi kusikia hivyo Penny lakini bado sijakufanyia kitu chochote kikubwa cha kuweza kunishukuru.Thi
s is just the beginning Penny.I’ll make you a Tanzanian queen.From now you are going to live like a queen” akasema Dr Joshua
“ Ahsante sana Dr Joshua.” Akasema Penny
“ Ok Penny.Najua nikiwa Dar es salaam nafasi yangu ya kuonana nawe itakuwa ndogo sana kutokana na kazi lakini nitajitahidi kadiri inavyowezekana kuonana nawe mara kwa mara ndiyo maana nimekuhamishia katika nyumba ambayo itakuwa rahisi kwangu mimi kufika mara kwa mara.Nisikucheleweshe Penny tutaongea mengi tutakapoonana Dar es salaam Jioni ya leo nitakuwa mgeni wako na kukupa habari njema ” akasema Dr Joshua
“ Ouh Dr Joshua ,you are so sweet.See you later” akasema Penny na kukata simu
“ Nimemchanganya sana huyu mzee kiasi kwamba hafikirii kitu chochote kingine zaidi yangu.Hahaha…the old man is deadly in love with me..Now that I can control him the way I want ,its time to finish my job.Kuna nyakati namuonea huruma sana huyu mzee kwa namna alivyokufa akaoza kwangu na kuwa tayari kufanya jambo lolote lile kwa ajili yangu,lakini sina namna nyingine ya kufanya zaidi ya kufanya kile ninachotakiwa kukifanya.” Akawaza Penny akiongozwa na walinzi wale wa rais kuelekea katika ndege maalum iliyoandaliwa kwa ajili ya kumrejesha Dar es salaam.Aliingia ndani ya ndege na kukaa,akafumba macho na kukumbuka mambo yote yaliyotokea jijini Arusha
“ Dr Joshua amejitahidi kufanya kila alichoweza ili kunifanya niwe na furaha. Nilivaa uhusika vizuri sana na kumfanya aamini kwamba nimefurahi na ninampenda.Yule mzee ananipenda sana na yuko tayari kufanya kitu chochote kunifanya niwe na furaha.Amenipatia jumba jipya pembeni ya bahari ili iwe rahisi kwake kufika katika muda wowote anaoutaka.Pamoja na yote haya anayoyafanya kwangu lakini si mtu wa saizi yangu.I don’t love him at all na toka ndani ya moyo wangu nina kisasi naye kikubwa sana kwa kumuua Edson kijana niliyempenda kwa moyo wangu wote.Ngoja niendelee kuuvaa uhusika hadi hapo mambo yangu yatakapotimia ndipo atakapogundua kwamba mimi si malaika kama anavyodhani” Akawaza Penny akiwa angani akielekea Dare s salaam
********
Baada tu ya kumaliza kuongea na Penny simuni,Dr Joshua akiwa amejifungia chumbani kwake akazitafuta namba Fulani katika simu yake na kutaka kubonyeza kitufe cha kupigia lakini akasita.Akaenda dirishani akatazama nje na kuzama katika mawazi kwa muda wa dakika kadhaa halafu akasema kwa sauti ndogo
“ let me do it”
Akabonyeza kitufe cha kupigia na kuiweka simu sikioni.Baada ya muda smu ikapokelewa
“ Captain Amos” akasema Dr Joshua
“ Hallo mheshimiwa “ akasema Captain Amos
“ Mgonja anaendeleaje?
“ Hali yake iko hivyo hivyo.Bado si nzuri .”
“ Ok Captain.Do it” akasema Dr Joshua.Kimya cha sekunde kadhaa kikapita Captain Amos akasema
“ Are you sure Mr President?
“ yes I’m sure.Do it. And Captain Amos,Thank you so much for this” akasema Dr Joshua na kukata simu.
Captain Amos aliyekuwa ni daktari wa familia ya rais akaegemea ukuta akawaza kwa dakika kadhaa halafu akachukua mkoba wake na kuelekea katika chumba cha mke wa rais,akagonga mlango ukafunguliwa na msaidizi wa mke wa rais
“ Muda wa matibabu sasa” akasema Captain amos na Yule msaidizi wa mke wa rais akatoka.
Captain Amos akachukua kichupa kidogo chenye dawa toka katika mkoba wake akainyonya dawa ile katika bomba la sindano na kumchoma mke wa rais
“ I’m sorry for this madam first lady” akasema Captain Amos na kutoka mle chumbani
********
Kwa muda wa dakika tatu Mathew aliendelea kusimama nje ya mlango wa kile chumba walichoingia wale jamaa.Alitamani ajue kilichokuwa kinaendelea mle ndani
“ Mathew talk to me” Anitha akasema
“ Anitha una hakika umesoma vizuri jina la mtu aliyemo ndani ya chumba hiki? Akauliza Mathew
“Chumba PV 2 – 78 amelazwa mgonjwa anayeitwa John Mwaulaya Albert.Kwani vipi Mathew.Unamfaha
mu mtu huyo?
Mathew akavuta pumzi ndefu na kusema
“ Yah ! Ninamfahamu.Kama ni kweli aliyemo ndani ya chumba hiki ni John Mwaulaya basi mambo si rahisi kama tunavyofikiri” akasema Mathew kwa sauti ndogo huku akiwa makini akiangalia kila upande kuhakikisha usalama wake kwani alikwisha anza kuhisi hatari eneo lile
“ Mathew who is this guy John Mwaulaya ? Akauliza Anitha
“ Anitha tutaongea baadae.Eneo hili si salama hata kidogo.Please stay in the car and don’t get out” akasema Mathew
“ Mathew whats going on? Akauliza Anitha.Mathew hakujibu kitu .Kuna watu wawili walikuwa wakija kwa kasi.
TUKUTANE SEHEMU IJAYO……SEASON 1
SEHEMU YA 20
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ Anitha una hakika umesoma vizuri jina la mtu aliyemo ndani ya chumba hiki? Akauliza Mathew
“Chumba PV 2 – 78 amelazwa mgonjwa anayeitwa John Mwaulaya Albert.Kwani vipi Mathew.Unamfaha
mu mtu huyo?
Mathew akavuta pumzi ndefu na kusema
“ Yah ! Ninamfahamu.Kama ni kweli aliyemo ndani ya chumba hiki ni John Mwaulaya basi mambo si rahisi kama tunavyofikiri” akasema Mathew kwa sauti ndogo huku akiwa makini akiangalia kila upande kuhakikisha usalama wake kwani alikwisha anza kuhisi hatari eneo lile
“ Mathew who is this guy John Mwaulaya ? Akauliza Anitha
“ Anitha tutaongea baadae.Eneo hili si salama hata kidogo.Please stay in the car and don’t get out” akasema Mathew
“ Mathew whats going on? Akauliza Anitha.Mathew hakujibu kitu .Kuna watu wawili walikuwa wakija kwa kasi.
ENDELEA………………………………..
Mathew alihisi wale jamaa wanamfuata ikamlazimu kuingia katika choo kilichokuwa chumba cha tatu kutoka kile chumba.Wale jamaa wawili waliouwa wakija kwa kasi wakaingia nao katika kile chumba alicholazwa John Mwaulaya.
“ Lazima nipate uhakika kama ni kweli mtu aliyelazwa mle ndani ni John Mwaulaya.Kama kweli ni yeye basi tutakuwa tumeingia katika hatari kubwa.” Akawaza Mathew akiwa amejificha chooni huku macho yake akiwa ameyaelekeza katika kile chumba cha John akitaka kufahamu kila kilichokuwa kikiendelea.
“ Mathew !.akaita Anitha
“ Hallow Anitha” akasema Mathew kwa kunong’ona
“ Say something.Whats going on over there? Akauliza Anitha
“ Anitha endelea kukaa ndani ya gari,bado ninaendelea kuwafuatilia hawa jamaa” akasema Mathew
“ Mathew mbona hutaki kunieleza nini kinachoendelea huko juu?
“ Anitha,nitakueleza lakini si sasa.” Akasema Mathew
Baada ya dakika kama thelathini hivi ,mlango wa kile chumba ukafunguliwa na jamaa wanne wakatoka wakiwa wameongozana na daktari mmoja wa kizungu
“ Anitha,wametoka watu wanne ndani ya kile chumba wameongozana na daktari mmoja wa kizungu.Nadhani wanashuka chini” Mathew akamtaarifu Anitha
“ Ok nitawaona katika kamera watakapofika chini” akasema Anitha
“ Tunamuhitaji Yule daktari wa kizungu.” Akaelekeza Mathew
“ Nimekusoma Mathew” akajibu Anitha
Mathew akatoka mle chooni alimokuwa amejibanza na kutembea kwa kasi akishuka chini kuwawahi wale jamaa.
“ Mathew tayari nimewaona wale jamaa katika kamera.Wako wanne na daktari mmoja wa kizungu.Wale jamaa wameagana na Yule dakatari ambaye kwa sasa anaongea na daktari mwenzake.Namuona Yule daktari ana kitambulisho katika koti lake .Ngoja nimvute karibu nifahamu jina lake” akasema Anitha
“ Ok Anitha.Achana na wale jamaa.Elekeza macho kwa daktari.Mimi niko ghorofa ya pili ninashuka ” akasema Mathew
Baada ya sekunde kadhaa Anitha akasema
“ I’ve got him !”
“ Anaitwa Michael Rodriguerz “
“ Good Job Anitha “ akajibu Mathew tayari akiwa ghorofa ya kwanza
Bado Dr Michael aliendelea kuongea na daktari mwenzake.Mathew akawapita halafu akaenda kusimama nje katika maua
“ Anitha niko hapa nje nikimsubiri atoke” akasema Mathew
“ Mathew , Dr James anatoka nje ya jengo anaelekea upande wa mashariki nadhani ndiko iliko ofisi yake” akasema Anitha
“ Ok Anitha nimekwisha muona,ninamfuatilia” akasema Mathew na kuanza kutembea taratibu akimfuata Dr Michael
“ Mathew nimetafuta kwa haraka haraka taarifa za Dr Michael ni kwamba ana umri wa miaka 53,ni mzaliwa wa Mexico,amesoma nchini Marekani ,Mexico na Urusi.Ni baba wa watoto watatu,Peter,Michael jr na Celine .Mke wake anaitwa Michelle Donalds mzaliwa wa Texas marekani.Dr Michael ni daktari bingwa wa mishipa ya fahamu” akasema Anitha
“ Thank you Anitha.Dr Michael sasa anaingia katika jengo lenye ofisi.Sintoweza tena kuingia mle ndani kwa sababu kuna kibao hapa kinachoonyesha kwamba huruhusiwi kuingia ndani kama si muhusika.Endele
a kumfuatilia kupitia kamera” akasema Mathew na kuanza kurudi mahala walikoegesha gari
“ John Mwaulaya !..” akawaza Mathew na mwili wote ukamsisimka
“ Bado siamini kama kweli ni yeye ndiye aliyelazwa ndani ya chumba kile hadi nitakapomtia machoni ndipo nitaamini” akawaza Mathew huku akitembea kwa kasi .Mara Anitha akaumuita
“ Mathew ,Dr Joshua ametoka,anaelekea katika eneo la kuegesha magari ya madaktari,anaingia katika gari lenye namba BV36P44.Umefika wapi ? akauliza Anitha
“ Tayari nimekwisha fika Anitha” akasema Mathew wakati akilikaribia gari lao.Alitembea kwa haraka akaufungua mlango na kuingia ndani
“ Ameelekea wapi? Akauliza Mathew huku akiwasha gari
“ Ameelekea geti la Mashariki”
“ Ok twende tuondoke tutamuwahi hapo bara bara kuu.” Akasema Mathew na kuwasha gari wakaondoka
Walisimama kwa dakika tatu kusubiri nafasi ya kuingia barabara kuu na mara Anitha akaliona gari la Dr Michael akamuonyesha Mathew
“ Ok.Nimemuona” akasema Mathew na kuingia barabarani akiacha magari matatu kati yao na Dr Michael
“ Hatupaswi kumpoteza.Tunamuhitaji sana” akasema Mathew
“ Mathew whats going on? Who is John mwaulaya? Nimejaribu kutafuta taarifa zake lakini hakuna mahala nimeweza kupata.Who is he? Akauliza Anitha
“ Tutaongea baadae Anitha lakini kwa sasa tuelekeze macho yetu kwa Dr Michael tusije tukampoteza.” akasema Mathew
“ Mathew tunaifanya kazi hii pamoja,na ili tufanikiwe tafadhali naomba uwe muwazi kwangu katika kila jambo ili tusaidiane mawazo nini cha kufanya” akasema Anitha
“ Usihofu Anitha.Kuna mambo mengi sana ambayo unahitaji kuyafahamu lakini kwa sasa tuyaweke pembeni na tuhakikishe hatumpotezi Michael” akasema Mathew.Anitha hakuuliza kitu tena wakaendelea na safari yao ya kumfuatilia Dr Michael.
Baada ya kutoka hospitali,Dr Michael alikwenda moja kwa moja Tanganyika Internationa school akaegesha gari na baada ya dakika kama tatu hivi ,mwanadada mmoja akatokea akiwa amemshika mkono mtoto mdogo .Dr Michael akamkumbatia Yule mtoto na kuwafungulia mlango wakaingia garini halafu wakaondoka.
“ Yule mtoto anaitwa Michael jr.Ni mtoto wa pili wa Dr Michael na Yule mwanadada aliyeongozana nao nadhani ni mtumishi wao” akasema Anitha
Waliendelea kumfuatilia Dr Michael bila ya yeye kufahamu kama anafuatiliwa.Toka pale shuleni Dr Michael hakupita sehemu nyingine ,alielekea moja kwa moja nyumbani kwake.Alipofika kwake alipiga honi akafunguliwa geti na kuingia ndani kisha geti likafungwa
“ Whats next ? akauliza Anitha
“ Najaribu kutafakari nini cha kufanya” akasema Mathew na mara mlango mdogo wa geti ukafunguliwa na Yule mwanadada aliyekuwa ameongozana na Dr Michael toka shuleni akatoka.
“ Yule dada anatoka.Amebeba mkoba wake inaonekana kama vile anaondoka” akasema Anitha
“ Go get her.We can use her .Tunahtaji kumpata Yule mtoto wa Dr Michael na itakuwa rahisi kama tukimtumia yeye” akasema Mathew.Anitha akashuka garini na kutembea kwa haraka akamfuata Yule dada ambaye alikuwa akitembea taratibu huku akiongea na simu.Mara tu alipomaliza kuongea na simu Anitha akamsalimu
“ Habari yako dada”
“ Habari yangu nzuri.Habari yako? Akasema Yule dada ambaye alikuwa na sauti laini ya upole
“ Naitwa Anitha,mwenzangu unaitwa nani? Akasema Anitha hukuakitabasamu
“ Naitwa Lydie Masawe” akasema
“ Nafurahi kukufahmu Lydie.Unaelekea wapi hivi sasa?
“ Naelekea nyumbani lakini nitapita kwanza saluni kurekebisha nywele na kucha”
“ Sawa Lydie,nadhani ni mara ya kwanza mimi na wewe kuonana”
“ Ndiyo ni mara ya kwanza dada Anitha.Sina kumbu kumbu kama tumewahi kuonana” akasema Lydie
“ Ok Lydie.Kama hutajali nina maongezi nawe kidogo kuhusu kazi.Sijui unaweza kuwa na nafasi sasa hivi? Au kama unaelekea uko saluni,nina usafiri wangu tunaweza tukaongozana na tukapata wasaa wa kuzungumza” akasema Anitha.Lydie hakuwa na wasi wasi wakaelekea mahala akina Mathew walikoegesha gari
“ Lydie huyu ni dereva angu anaitwa Mathew” Anitha akafanya utambulisho mfupi baada ya kuingia garini
“ Mathew tupeleke Zulphat beauty salon” akaelekeza Anitha.
Ndani ya gari walikuwa wakiongea mambo mbali mbali yahusuyo urembo kwa ujumla hadi walipowasili Zulphat beauty salon moja kati ya saluni kubwa za akina mama jijini Dar.Lydie alitengenezwa kwa gharama za Anitha kwani saluni hii ni moja kati ya saluni zenye gharama kubwa.Baada ya hapo wakaelekea Ibona hotel kwa ajili ya maongezi
“ Lydie nimekuleta hapa ili tuweze kuongea kwa utulivu na nafasi” akasema Anitha wakiwa katika bustani tulivu
“ Nakusikilza dada Anitha”
“ Lydie umeolewa? Akauliza Anitha ili kutaka kumfahamu vizuri
“ Hapana bado ila nina mtoto mmoja”
“ Hongera.Mwanao yuko wapi? Akauliza Anitha
“ Yuko kwa babu yake huko Moshi”
“ Kwa nini usimchukue ukaishi naye?
“ Natamani sana kufanya hivyo lakini hali ngumu ya maisha inanilazimu nimuache kwa babu zake”
“ Sawa nimekuelewa Lydie.Sasa dada yangu bila kupoteza wakati nimekufuata nina kazi moja ambayo nahitaji unifanyie.Endapo utakubali basi unaweza ukapata pesa ambayo itakusaidia sana katika kuondokana na maisha haya duni na ukaanzisha biashara zako mwenyewe na hutafanya tena kazi kwa mtu na utakuwa na uwezo wa kuishi na mwanao na kumpatia elimu bora ” akasema Anitha
“ Nitashukuru sana dada Anitha kama utanipatia kazi ambayo itaniwezesha niweze kupata mtaji wa kujiajiri mwenyewe.Niambie ni kazi gani unataka nikufanyie? Una mtoto wa kulea?”
“ Hapana sina mtoto bado Lydie lakini kuna kazi nyingine ndogo tu tena ya masaa machache.Kwanza nieleze pale kwa Dr Michael unafanya kazi gani?
“ Kazi yangu ni kumlea Michael Jr.Asubuhi kumuandaa na kumpeleka shule ambako huwa nikishinda huko hadi saa nane mchana.Dereva huja kutuchukua na kuturudisha nyumbani.Saa tisa kamili ndiyo mwisho wangu wa kazi na hurejea nyumbani” akasema Lydie
“ Ok Lydie sasa ni hivi,kuna taarifa muhimu sana tunayoihitaji toka kwa Dr Michael na ambayo hawezi kutupatia hivi hivi,kwa hiyo tunahitaji kutumia njia mbadala kuipata taarifa hiyo.Nahitaji kumtumia mtoto wake Michael kumtisha kidogo ili aweze kunipatia taarifa hiyo” akasema Anitha na kumtazama Lydie
“ Wewe ni polisi? Akauliza Lydie kwa wasi wasi
“ Hapana,mimi si polisi lakini kazi zangu zinafanana kidogo na za polisi.” akajibu Anitha
“ Kwa hiyo unataka kumtumiaje Michael Jr?
“ Nitamtumia kama chambo ili niweze kuipata taarifa ninayoitaka toka kwa Dr Michael.Najua anampenda sana mwanae hivyo akisikia kwamba mtoto wake yuko mikononi mwangu lazima atatoa taarifa hiyo ninayoitaka” akasema Aitha.Lydie akaonekana kuogopa sana
“ Dada Anitha naona siwezi kuifanya hiyo kazi.Ni kazi ya hatari sana na inaweza kunisababishia matatizo.Hilo ni kosa kubwa na endapo nikishikwa na polisi nitaweza hata kufungwa kwa kosa la utekaji na mwanangu akabaki akiteseka.Utanisamehe dada yangu sintoweza”
Anitha akatabasamu kidogo na kusema
“ Usiogope Lydie.Suala hili haliwezi kwenda polisi kwa sababu mimi ninafanya kazi kwa niaba ya polisi kwa hiyo hata kama likifika kwao wananifahamu kwamba niko kazini na lengo langu si kumuumiza mtoto huyo wala Dr Michael,bali ni kupata taarifa hiyo muhimu sana kwa usalama wa taifa.”
“ Pamoja na hayo dada Anitha bado naona sintoweza.Sijawahi kufanya kazi kama hiyo hata mara moja,zaidi ya yote familia ile wananipenda na kunihudumia vizuri ,siwezi kuwafanyia kitendo kama hicho” akasema Lydie.Anitha akamtazama kwa sekunde kadhaa na kumuuliza
“ Lydie unatoka katika mkoa wa Kilimanjaro,si ndiyo?
“ Ndiyo”
“ Ninawafahamu watu wa Kilimanjaro hususani wanawake ni watafutaji wazuri wa pesa.Ni wapambanaji wa kweli katika kutafuta maisha.Wanaitafuta pesa bila kuchoka na hawaogopi changamoto zilizoko mbele yao na hiyo ndiyo siri ya wao kufanikiwa sana.Tunawaona wengi hapa Dar es salaama namna walivyofanikiwa ,namna walivyochangamka kuitafuta pesa,hawakuja hapa mjini kutazama maghorofa au kuza sura zao nzuri,bali wamekuja kutafuta pesa.Ninakupa fursa ya kujikwamua kiuchumi naomba usiipuuze.Please Lydie wake up.This is your chance.Vaa uhusika wa mwanamke wa kichaga asiye ogopa changamoto na ukubali kuifanya kazi hii ndogo lakini yenye maslahi manono.Niambie unahitaji kiasi gani nikupatie? Akauliza Anitha.Lydie akainama akafikiri
“ Ok ngoja nikutajie .Mimi nitakupa Tsh Milioni saba ili uweze kunifanyia kazi hiyo” akasema Anitha na mara Lydie akainua kichwa
“ Kiasi hicho kiko tayari?
“ Ndiyo kipo tayari.Uko tayari kuifanya kazi hii?
“ Kama mtanilipa kiasi hicho cha pesa mimi niko tayari lakini kwa sharti moja tu kwamba mnipatie kwanza kabla sijawafanyia kazi hiyo kwa sababu ninaweza nikahatarisha usalama wangu halafu msinilipe chochote nikawa nimeharibu kazi yangu na maisha yangu”
“ Usihofu kuhusu pesa hata sasa hivi unaweza ukapewa mradi tu ukubali kuifanya hiyo kazi” akasema Anitha
“ Mimi niko tayari kuifanya.Si umesema suala hili haliwezi kufika polisi?
“ Ndiyo haliwezi kufika polisi”
“ Ok nielekeze unataka nifanye nini?
“ Asubuhi utampeleka Michael Jr shule kama kawaida.Saa tano za asubuhi tutakuja na gari na utawaambia waalimu kwamba umepigiwa simu uwahi kurejea nyumbani.Utatukabidhi mtoto na tutakukabidhi mzigo wako na utapotea na huo utakuwa ni mwisho wako kufanya kazi pale kwa Dr Michael.Sisi tutakaa na Yule mtoto kwa masaa machache na Dr Michael atakapotupatia taarifa yetu basi tutampatia mtoto wake.Nakuhakikishia tena kwamba hatuna lengo la kumdhuru mtoto wala mtu yeyote” akasema Anitha.Wakakubaliana na Lydie halafu wakaagana
“ Amekubali japo haikuwa rahisi kumshawishi.Imenilazimu kumtajia dau kubwa ndipo akakubali.Tutamlipa Tsh Milioni saba.” Akasema Anitha baada ya kuachana na Lydie na yeye kurejea garini alikomuacha Mathew
“ Good.Una hakika hawezi kutusumbua au kutuletea matatizo? Akauliza Mathew
“ She wont.She needs money.” Akajibu Anitha
“ Ok Good.Noah amenipigia simu tayari amekwisha wasili.Timu imekamilika” akasema Mathew
“ Wow that’s great.So whats next?
“ Kwa sasa tunatakiwa kuwasiliana na Elibariki ili tumfahamishe kuhusiana na pesa hii ili watupatie au kama hawana basi tutatumia za kwangu na wataturejeshea.Hatuwezi kukwama kwa sababu ya pesa” akasema Mathew
*********
Eugenia Conrad,msaidizi wa Dr Flora Johakim mke wa rais,alitoka mbio ndani ya chumba cha Dr Flora huku akipiga kelele. Walinzi walimkamata na kumuuliza kulikoni kupiga kelele zile
“ Mama Flora !!....Mama Flor……………!!!” hakumaliza sentensi yake akaanguka na kupoteza fahamu.Koplo Winifrida mlinzi wa Dr Flora akakimbia hadi chumbani kuangalia kuna nini,na ghafla akahisi miguu inamuisha nguvu.Dr Flora Johakim mke wa rais alikuwa amelala kitandani huku damu zikimtoka mdomoni na puani.Akajikaza na kukisogelea kitanda na kuita
“ Dr Flora.!!,Dr Flora !!....
Dr Flora hakutikisa hata ukope.Haraka haraka Winifrida akakimbilia katika simu akampigia Captain Amos daktari wa familia ya rais ambaye alifika mara moja na vipimo akampima na kuamuru liitwe gari la wagonjwa haraka.Gari la wagonjwa likafika Dr Flora akapakiwa na kukimbizwa katika hospitali ya jeshi.Pale akapimwa na kukutwa tayari amekwisha fariki.Baada ya kuthibitishwa kwamba amefariki dunia Captain Amos akampigia simu Dr Joshua
“ Hallow Captain” akasema Dr Joshua
“ Mr President its done.She’s dead”
“ Thank you Captain Amos.Niko njiani narejea Dar es salaam” akasema Dr Joshua na kukata simu.Captain Amos alibaki amesimama ameegemea mti.Alikuwa na mawazo mengi sana.
“ I’ve killed the first lady…Please forgive me lord” akawaza Captain Amos
TUKUTANE SEHEMU IJAYO………………
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad

Hollywood Movies