🔥🌹
SEASON 1
SEHEMU YA 11
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ Toka nimezaliwa hata baba yangu hajawahi kunipiga kofi sembuse wewe ng’ombe ! ..Kauli ile ikampandisha hasira Elibariki na kuanza kumshushia mke wake kipigo kikali kilichomfanya apige ukelele mkubwa .Jaji Elibariki hakujali kelele zile akaendelea kumpa kipigo mkewe.Hadi anamuachia Flaviana alikuwa anavuja damu.
“ Siku nyingine usithubutu kabisa kunidharau paka wewe ..! akasema jaji Elibariki huku akitweta kwa hasira Huku akilia,Flaviana akaingia bafuni na kujifuta damu zilizotoka katika majeraha yaliyotokana na kipigo kikali
“ Eli umenipiga hadi kunitoa damu.Sasa nitakuonyesha mimi na wewe nani mwenye nguvu.I swear in heaven and earth lazima nikuonyeshe kazi na hautanisahau mpaka unaingia kaburini”akasema kwa hasira flaviana na kutoka kwa kasi akaingia katika gari lake na kuondoka kwa kasi
“ Nimechoshwa na dharau za familia hii.Yote hii ni kwa sababu baba yao ni rais .Hapana hawawezi kunitisha hata kidogo,hakuna aliye juu ya sheria.” Akasema jaji Elibariki kwa hasira.
ENDELEA…………………………
Jaji Elibariki alikaa kitandani na kuanza kutafakari maisha yaketoka alipokutanana Flaviana ,wakapendana,wakwa wachumbanabaadae wakafungandoa.Aliyatafakari maisha yake ya ndoa toka walipooana hadi leo hii
“ Sina hakika kama tuliingia katika ndoa tukiwa tumejiandaa vya kutosha.Sina hakika kama tulikuwa na mapenzi ya kweli au zilikuwa ni tama tu za ujana.Toka tumeyaanza maisha yandoa hakuna amanindani mwetu.It’s been a living hell to me.Tukiwa nje tunaonekana ni watu wenye mapenzi mazito lakini hajuna ajuaye siri yetu ya ndani.Maisha yetu yamejaa mifarakano,dharauna ugomvi.Nimechoshwa na maisha haya.Nimechoka kuwadanganya watu kwamba tunapendana kwa dhati wakati si kweli.Nadhani ni wakati muafaka sasa wa kufanya maamuzi na kila mmoja wetu akatafute furaha ya maisha yake.Siwezi kuendelea na maisha kama haya” akawaza halafu akaenda katika kabati dogo lililokuwa mle chumbani akalifunguana kutoa chupa ya mvinyo akajimiminia katika glasi akanywa na mara sura a Peny ikamjia kichwani “ Penny !!..akasema kwa sauti ndogo huku akitabaamu
“ Mwanamke kama Penny anafaa sana kuwa mke.Aba uzuri wa kipekee ambao sioniwa kumfaanisha naye na ana adabu na hata ukiongea naye utabaini wazi kwamba ni mwanamke mqwnye heshima kubwa/Jaji Elibarikiakaendelea kuwaza na mara akastuliwa namlio wa simu.Akaichukuana kutazmaa mpigaji ,alikuwa ni baba mkwe wake Dr Joshua,rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania.
“ Kazi imeanza” akasema kimoyo moyo na kubonyeza kitufe cha kupokelea simu
“ Hallo mzee shikamoo”
“ Marahaba mheshimiwa jaji,habari za kwenu?
“ Habari nzuri tu mzee,sijui ninyi huko”
“ Sisi wazima.Eli uko wapi?
“ Niko nyumbani mzee”
“ Ok vizuri.Nakuomba hapa ikulu sasa hivi nina maongezi nawe” akasema Dr Joshua na kukata simu
“ Flaviana amekwenda kunishitaki kwa baba yake akidhani labda nitamuogopa.Sintomuogopa mtu yeyote hata kama ni rais wan chi.Kuanzia sasa yeyote atakayenidharau kwa namna yeyote ile nitapambananaye” akawaza huku akivaa koti na kutoka kueleka ikulu kuonana na baba mkwe wake. Ilimchukua dakika zaidi ya hamsini kuwasili katikamakazi ya rais.Baada ya kama dakika kumi na tatu toka awasili ,Dr Joshua akajitokeza sebuleni.Jaji Elibariki akasimama wakasalimiana “ Mheshimiwa jaji ,hebu nieleze nini kimetokea huko kwenu na kusababisha umpige mwenzako na kumuumiza kiasi kile? Akaanzisha mazungumzo Dr Joshua.Elibariki akavuta pumzi ndefu na kisha akamsimulia rais kila kitu kilichotokea na kusababisha apandwe na hasira na kumpiga mkewe.
“ Nimekuelewa Elibariki ,lakini pamoja na yote aliyoyafanya mwenzako ulitakiwa ujizuie, hukupaswa kufikia hatua ya kumpiga mwenzako namna ile.Migongano ndani ya nyumba ni kitu cha kawaida na suluhisho lake ni kukaa mkaongea mkayamaliza na si kurushiana makonde.Wewe kama kichwa cha nyumba unahitajika uwe na busara ya hali ya juu “ akasema Dr Joshua
“ Nakuelewa mzee,lakini nilifikia maamuzi ya kumpiga kidogo mke wangu kutokana na dharau alizoniletea.Kama nilivyokueleza mzee ni muda mrefu sasa amekuwa akinidharau sana na leo hii uvumilivu ulinishinda nikaona bora nimuonye kidogo” akasema Elibariki “ Siku nyingine endapo atakuletea dharau na kiburi,wasiliana nami moja kwa moja kabla ya kuchukua maamuzi ya kumpiga.Sipendi sana kuona mwanangu yeyote akilia machozi na hasa ya kupigwa na mwanaume” akasema Dr Joshua
“Lakini mzee, Flaviana ni mke wangu na mambo yetu yanndani tunayamaliza wenyewe.Haitapendeza kila siku niwe nakupigia simu na kukwambia kwamba mwanao amenidharau.Naomba mzee utuachie mambo yetu ya ndani tuyamalize sisi wenyewe.” Akasema Elibariki
“Kuyamaliza kwa staili hii ya kutoana damu? No !.. Sitaki kabisa mwanangu aguswe tena na kutolewa damu.Usinione ninaongea nawe hapa lakini nimechukizwa mno na kitendo ulichokifanya leo cha kumpiga mwanangu.Naomba kisijirudie tena.Marufuku kumfanya mwanangu sehemu ya mazoezi” akasema Dr Joshua kwa sauti ya juu yenye amri ndani yake .Jaji Elibariki akakereka sana kwa maneno yale ya baba mkwe wake
“ Lakini mzee………….” Akataka kusema jambo ,akazuiwa na Dr Joshua
“ Hakuna cha lakini…..Nimesema sitaki mwanangu aguswe and that’s fnal.Sitaki tena mjadala.Hata akikukosea vipi sitaki umpige.Nieleze mimi mwenyewe nitaongea naye” akasema kwa ukali Dr Joshua “ lakini mzee huyu ni mke wangu na amekuwa akinifanyia mambo mengi ya dharau ambayo siwezi hata kukueleza.Unapoongea maneno kama hayo unampa nguvu ya kufanya anachokitaka kwangu kwa kuwa anajua baba yake anamtetea” akalalamika Elibariki.Dr Joshau akasimama na kumsogelea “ I’m her father and I’m warning you….” Akasema Dr Joshua.maneno yale yakamkera sana Elibariki naye akasimama. “ Yes 1 you are her father but I’m her husband !!.... akasema Elibariki kwa sauti ya juu kidogo.
“ Elibariki,tafadhali chunga sana maneno unayoongea mbele yangu.Wewe bado hauna uwezo wa kusimama na kubishana na mimi.Ukumbuke kwamba ni mimi ndiye niliye kutoa huko maporini na kukupandisha hadi hapa ulipo.kwa hiyo kuwa makini sana siku nyingine unapoongea na mimi.Nina uwezo wa kukufanya chochote kile” akafoka dr Joshua.Elibariki akamtazama kwa macho makali na kusema
“ Naomba unisikilze mzee.Nimechoshwa na wewe na wanao kila mara kunisimanga kutokana na cheo hiki.Naomba mfahamu wewe na wanao kwamba cheo hiki hukunipa wewe bali nimepewa na Jamhuri ya muungano wa Tanzania na nimepewa kwa sababu ninafaa na nina vigezo vyote vya kuwepo hapa nilipo.Kwa maana hiyo naomba muache kuanzia sasa kunisakama kuhusiana na cheo hiki.Kitu kingine mnachotakiwa kukifahamu ni kwamba ofisi hii si mali ya familia,kwa hiyo si wewe wala wanao mnaoweza mkanishinikiza nifanye kazi yangu kwa matakwa yenu.Ninaifanya kazi yangu kwa mujibu wa sheria za nchi na si kwa kumfurahisha mtu Fulani..”akasema kwa ukali na kutoka kwa hasira akimuacha Dr Joshua akishangaa.
“ Nimemueleza ukweli wake,akichukia shauri lake,nimechoshwa na dharau zao” akawaza Elibariki huku akiingia katika gari lake na kuondoka
“ Kichwa changu kimevurugwa kabisa na Yule mzee.I need someone to talk to.I need some comfort” akawaza na mara sura ya penny ikamjia
“ penny !!... I need to talk to her.pengine kichwa changu kinaweza kutulia” akapunguza mwendo wa gari akatoa simu na kuzitafuta namba za Penny ,akapiga lakini haikuwa ikipatikana.
*********
Asubuhi na mapema jaji Elibariki aliamka na kufanya mazoezi ya viungo halafu akajianda na kuondoka.Flaviana hakurejea nyumbani usiku toka alipoondoka
“ Nadhani huu utakuwa ni mwanzo wa maisha mapya.Sina hakika kama kuna suluhu yoyote itapatikana tena baina yangu na Flaviana.Ni wakati sasa wa kuanza kuitafuta upya furaha ya moyo wangu ambayo nilitegemea kuipata kwa Flaviana lakini kumbe nilikuwa najidanganya.Nimeambulia karaha badala ya raha.Toka nilipomuoa hadi hivi leo hata mtoto amekataa kunizalia kwa kisingizo cha kutokuwa tayari.Hapana imetosha sasa.Maisha haya lazima yafikie mwisho.Kwa sasa ngoja kwanza nielekeze nguvu kumtafuta muuaji wa Edsoni ili Penny aweze kuwa salama” Mara tu alipomkumbuka Penny,akatabasamu na kutoa simu yake akazitafuta namba za Penny akapiga lakini bado simu yake haikuwa ikipatikana.
“ Ameamua kuizima simu yake,inawezekana hataki usumbufu toka kwa watu.Ametoka katika matatizo makubwa na anahitaji muda wa kukaa mwenyewe atafakari maisha yake bila usumbufu toka kwa watu” akawaza Jaji Elibariki Moja kwa moja alielekea Mandarini Hotel mahala ambako hupenda sana kwenda kupata kifungua kinywa.
“ Watu wengi wananishangaa ni kwa nini mtu kama mimi,Jaji wa Mahakam kuu ninakuja kupata kifungua kinywa hotelini? Hawajui Kero nilizonazo katika ndoa yangu.lakini soon mambo yote haya yatakwisha and I’ll be happy again.” Akawaza wakati akiendelea kupata kifungua kinywa. Toka Mandarin hotel,akaelekea ofisini kwake ambako hakukaa sana akatoka akaelekea mahala alikopanga akutane na Mathew.
TUKUTANE SEHEMU IJAYO…
PENIELA
SEASON 1
SEHEMU YA 12
ILIPOISIA SEHEMU ILIYOPITA
Mara tu alipomkumbuka Penny,akatabasamu na kutoa simu yake akazitafuta namba za Penny akapiga lakini bado simu yake haikuwa ikipatikana
“ Ameamua kuizima simu yake,inawezekana hataki usumbufu toka kwa watu.Ametoka katika matatizo makubwa na anahitaji muda wa kukaa mwenyewe atafakari maisha yake bila usumbufu toka kwa watu” akawaza Jaji Elibariki Moja kwa moja alielekea Mandarini Hotel mahala ambako hupenda sana kwenda kupata kifungua kinywa. “ Watu wengi wananishangaa ni kwa nini mtu kama mimi,Jaji wa Mahakam kuu ninakuja kupata kifungua kinywa hotelini? Hawajui Kero nilizonazo katika ndoa yangu.lakini soon mambo yote haya yatakwisha and I’ll be happy again.” Akawaza wakati akiendelea kupata kifungua kinywa. Toka Mandarin hotel,akaelekea ofisini kwake ambako hakukaa sana akatoka akaelekea mahala alikopanga akutane na Mathew.
ENDELEA……………………………..
Dakika kumi baada ya kuwasili Malaika Lounge mahala walikopanga wakutane na Mathew,Jason akawasili, wakasalimiana akavuta kiti na kuketi
“ Jason” akaanzisha mazungumzo Jaji Elibariki
“ kama nilivyokueleza simuni ,nimefikiria sana kuhusiana na jambo tunalotaka kulifanya na kuona ugumu wake .Sisi tumebobea katika masuala ya sheria na hatuna taaluma yoyote ya kufanya uchunguzi.Ni kwa sababu hii nimelazimika kumtafuta Mathew Kwanga” akanyamaza kidogo ,akamtazama Jason na kuendelea.
“ Mathew Kwanga aliwahi kufanya kazi katika idara ya ujasusi ya taifa na aliacha kazi hiyo baada ya familia yake yote kuteketezwa kwa moto.Kwa hivi sasa yeye ni mtu anayekodishwa na mataifa kazi za siri za kiuchunguzi .Ni mtu aliyebobea mno katika kazi hizi .Nina imani atatufanyia kazi nzuri “ akasema Jaji Elibariki
“Umefanya jambo la msingi sana mheshimiwa jaji.Hata mimi nilikuwa nafikiria kukushauri tufanye kitu kama hicho.Sisi peke yetu hatuwezi kulifanikisha jambo hili .Tunahitaji msaada wa mtu mwenye uzoefu wa kutosha na mambo haya.Natumai Mathew ni chaguo sahihi na atakuwa na msaada mkubwa sana kwetu” akasema Jason
“ Exactly !...Thats my point..Mathew ni mtu ambaye tumefahamiana kwa muda refu na sina shaka yoyote na uwezo wake.Ni mtu mwenye uwezo wa hali ya juu sana.By the way how’s Peniela? Akauliza Jaji Elibariki.Jason akaguna kidogo na kusema
“ Siku ya pili sasa hapatikani simuni”
“ May be she needs sometime alone. Unajua ametoka katika matatizo makubwa kwa hiyo yawezekana akahitaji kuituliza akili yake bila bughudha za watu.Let’s give her sometime” akasema Jaji Elibariki na mara Mathew akatokea.Alikuwa ni kijana nadhifu aliyevaa suti nzuri iliyompendeza
“ Hallo gentlemen…” akasema Mathew huku akipeana mikono na akina Jason
“ Mathew kutana na Jason,wakili maarufu sana hapa Tanzania.” Bila kuchelewa Jaji Elibariki akaanza kutoa utambulisho
“ Jason kutana na Mathew Kwanga.Ni rafiki yangu wa siku nyingi na mtu aliyebobea katika masuala ya kiuchunguzi”
Jason na Mathew wakashikana mikono kwa kujuana
“ Mtanisamehe sana ndugu zangu kwa kuchelewa .Nilipatwa na dharura ya ghafla” akasema Mathew
“ Usijali Mathew.Hakuna kilichoharibika.Nadhani umelifanyia kazi lile suala letu” akasema Jason
“ Ndiyo mheshimiwa Jaji.Nimejaribu kutafakari kwa kina kuhusiana na kazi mliyonipa na namna nitakavyoweza kuifanya.Naomba niwaweke wazi kwamba kazi hii si ndogo kama mnavyoifikiria. Edson alikuwa mfanyakazi katika kitengo cha habari Ikulu,huyu si mtu mdogo kama watu wanavyoweza kudhani.Ninashawishika kuamini kwamba lazima aliuawa kwa sababu maalum.Kazi yetu ni kuitafuta sababu hiyo iliyopelekea yeye kuuawa pamoja na watu waliomuua na kesi kumuangukia Peniela.Kazi hii si nyepesi lakini nawaahidi kwamba hakuna yeyote ambaye alikuwa na mkono wake katika mauaji hayo atabaki salama.Nitawatafuta katika kila pembe ya nchi hii na dunia mpaka nihakikishe nimewatia mikononi wale wote waliofanya kitendo hicho cha kinyama na mzigo wote wakamuangushia Penny.” akanyamaza kidogo na kuendelea
“ Kabla hatujaendelea mbele zaidi naomba tukubaliane kwanza kitu kimoja.kazi hii ni ya gharama kubwa.Kabla sijaingiza mguu wangu katika uwanja wa mapambano nahitaji kufahamu kama mtakuwa tayari kwa gharama za shughuli hii japokuwa haitakuwa kubwa kwani ninaifanya tu kwa ajili ya ninyi ndugu zangu lakini sikuwa nataka kufanya kazi yoyote hapa nyumbani.” Akasema Mathew.Jason na Jaji Elibariki wakatazamana na Jason akasema
“ Tuko tayari Mathew.Usihofu kuhusu gharama”
“ Ok Good.Sasa tunaweza kuendelea” akasema Mathew.
“ Katika kazi hii pia nitashirikiana na watu wawili.Wa kwanza ni Anitha Monera na wa pili ni Noah Ikuso.” Akasema Mathew huku akiwapa akina Jason mafaili ya watu hao wayapitie
“ Anitha Monera ana miaka ishirini na tisa.Ni mtanzania anayeishi nchini Marekani.Huyu ninamuita ni mchawi wa kompyuta. Anaichezea kompyuta kwa kiasi cha kushangaza .Nimekuwa nikimtumia sana katika kila kazi ninayoipata na siwafichi ndugu zangu huyu amekuwa ni msaada mkubwa kwangu na ndiye amenifanya nifanikiwe katika kila kazi ninayopata” akanyamaza kidogo na kuendelea
“ Noah ikuso naye ni mtanzania pia.Ana umri wa miaka thelathini na tatu .Aliwahi kufanya kazi katika idara ya usalama wa taifa .Ni kijana mahiri na hodari katika kazi.Ninao wengi ambao ninaweza kufanya nao kazi hii lakini nimewachagua hawa wawili ambao naamini wanatosha sana kuikamilisha hii kazi kwa umahiri na haraka” akasema Mathew.Jason na jaji Elibariki waliendelea kupitia mafaili ya vijana wale halafu Jason akasema
“ Kwa upande wangu sina kipingamizi chochote.Kama unawaamini vijana hawa kwamba wanaweza kazi basi unaweza kuwatumia”
“ Yah ! ninawaamini sana.Ni mahodari na hawana mchezo katika kazi.” Akasema Mathew,kikapita kimya kifupi akauliza
“ Kuna kitu kimoja bado hamjaniweka wazi.Nina hakika nitawapata watu hawa waliofanya kitendo hiki,lakini je wakipatikana nini kitafuata? Wanashughulikiwa vipi? Au mtawakabidhi katika mikono ya dola?
“ Lengo letu sisi ni kuwafichua na kuwakabidhi katika mikono ya dola.Kitu kikubwa kinachonisukuma mimi na mwenzangu tuwe tayari kugharamia jambo hili ni kuudhihirishai umma wa watanzania kwamba sikufanya maamuzi ya kukurupuka kumuachia huru Peniela.Nataka watu wawe na imani na mahakama kwamba ndicho chombo pekee chenye kutenda haki bila kujali mtu.Hatuna lengo la kulipiza kisasi,bali tukimbaini muuaji tutamfikisha katika mikono husika na sheria itachukua mkondo wake na sisi tutabaki salama.” Akasema Jaji Elibariki
“ Ok sasa nimekuelewa mheshimiwa jaji.usijali watapatikana tu.Kitu kingine ninachohitaji ni kumpata Peniela ili niweze kuongea naye mawili matatu kwani yeye ndiye aliyekutwa eneo la tukio.Nataka niyafahamu mazingira ya tukio namna yalivyokuwa.” akasema Mathew
“ Peniela leo ni siku ya pili simu yake haipatikani na sijui yuko wapi.” Akasema Jason
“ Are you sure she’s ok? Akauliza Mathew
“ Sina hakika sana kwa sababu jana nilikwenda nyumbani kwake lakini getini kulikuwa na makufuli na ilionyesha wazi kwamba hakukuwa na mtu ndani”
“ Ok Vizuri.Wakati tukimsubiri nitaanza uchunguzi wangu kwa Edson.Ninataka mnielekeze mahala alipokuwa akiishi na baada ya hapo mtaendelea na kazi zenu kama kawaida na mimi nitaendelea na kazi yangu,popote nitakapokwama na kuhitaji msaada wenu nitawaambia” akasema Mathew.Wakaendelea na kikao chao na kupeana maelekezo kadhaa halafu Jason na Mathew wakaeleekea mahala alipokuwa akiishi Edson.
“ Umeshawahi kuonana na huyo kijana Edson? Akauliza Mathew wakiwa garni
“ Hapana sijawahi kuonana naye hata mara moja”
“ Umewahi kuingia ndani mwake?
“ Ndiyo nimeingia mara moja tu wakati kesi ikiendelea.Kuna wakati iliilazimu mahakama ihamie hapa kuthibitisha madai ya upande wa mashtaka.”
“ Ok Good.” Akasema Mathew na safari ikaendelea.
Jason akaegesha gari nje ya nyumba aliyokuwa akiishi Edson
“ Ni hapa” akasema.Mathew akaitazama nyumba ile halafu akashuka na kumuomba Jason amsubiri garini.Akaelekea getini akabonyeza kengele ya getini na baada ya dakika moja mlango mdogo wa getini ukafunguliwa akatoka kijana mmoja .
“ Habari yako ndugu”
“ Habari yangu nzuri.Karibu sana.Nikusaidie nini? Akauliza Yule kijana
“ Samahani ndugu yangu.Nimemkuta Edson? Akauliza Mathew
“ Edson?!.. yule kijana akashangaa
“ Ndiyo Edson.”
“ Yawezekana umekosea nyumba.Hakuna Edson anayeishi humu ndani”
“ Yawezekana nimekosea .Ninaishi nje ya nchi na mara ya mwisho nilipokuja huku Tanzania Edson alinileta hapa mahala alipokuwa anaishi na ndiyo maana nimekuja moja kwa moja hapa.Yawezekana nimepotea nyumba lakini kumbukumbu zangu zinaniambia ni hapa hapa.” Akasema Mathew
“ Anafanya kazi wapi huyo Edson? Pengine naweza kukusaidia kumtafuta “ akasema Yule kijana
“ Edson anafanya kazi ikulu” akajibu Mathew
Yule kijana akamtazama Mathew kwa mshangao kidogo na kuuliza
“ Mara ya mwisho mliwasiliana lini ?
“ Nina zaidi ya mwaka sasa sijawasiliana naye”
“ Dah ! pole sana kaka.Kama unamuongelea huyo kijana aliyekuwa akifanya kazi ikulu ni kweli alikuwa akiishi hapa lakini inasemekena aliuawa na ndiyo maana wazazi wake wakaamua kuiuza nyumba hii”
Mathew akaonyesha mstuko mkubwa.
“ Dah sikuwa na taarifa hizo.Ahsante sana kwa taarifa hizo ndugu yangu.Nitakwenda kuwapa pole wazazi wake” akasema Mathew na kurejea garini.
“ Wazazi wa Edson wamekwisha iuza nyumba hii .Kwa maana hiyo vitu vyote vya Edson viliondolewa hapa na nina hakika vilipelekwa nyumbani kwa wazazi wake.Nahitaji kukagua vitu vyake.Nahitaji kuikagua simu aliyokuwa akiitumia na kompyuta yake kama bado vipo.“ akasema Mathew
“ Kama ni hivyo itatulazimu kwenda nyumbani kwa wazazi wake na kuonana nao na kuwaomba kupitia vitu hivyo” akasema Jason
“ Hiyo ndiyo hatua inayofuata.Unafahamu mahala wanakoishi wazazi wake?” Akasema Mathew.
“ Ndiyo ninapafahamu.Baba yake ni mtu maarufu sana hapa mjini..” akasema Jason..
“ Ok.Kama tukionana na wazazi wa Edson tukaongea nao tunaweza kupata japo sehemu ya kuanzia.” Akasema Mathew.
TUKUTANE TENA SEHEMU IJAYO………
SEASON 1
SEHEMU YA 13
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ Dah ! pole sana kaka.Kama unamuongelea huyo kijana aliyekuwa akifanya kazi ikulu ni kweli alikuwa akiishi hapa lakini inasemekena aliuawa na ndiyo maana wazazi wake wakaamua kuiuza nyumba hii”
Mathew akaonyesha mstuko mkubwa.
“ Dah sikuwa na taarifa hizo.Ahsante sana kwa taarifa hizo ndugu yangu.Nitakwenda kuwapa pole wazazi wake” akasema Mathew na kurejea garini.
“ Wazazi wa Edson wamekwisha iuza nyumba hii .Kwa maan hiyo vitu vyote vya Edson viliondolewa hapa na nina hakika vilipelekwa nyumbani kwa wazazi wake.Nahitaji kukagua vitu vyake.Nahitaji kuikagua simu aliyokuwa akiitumia na kompyuta yake kama bado vipo“ akasema Mathew
“ Kama ni hivyo itatulazimu kwenda nyumbani kwa wazazi wake na kuonana nao na kuwaomba kupitia vitu hivyo” akasema Jason
“ Hiyo ndiyo hatua inayofuata.Unafahamu mahala wanakoishi wazazi wake?” Akasema Mathew.
“ Ndiyo ninapafahamu.Baba yake ni mtu maarufu sana hapa mjini..” akasema Jason..
“ Ok.Tunaweza kupata japo sehemu ya kuanzia.” Akasema Mathew.
ENDELEA………………………………………………….
Jason na Mathew wakawasili katika makazi ya wazazi wa Edson.Lilikuwa ni jumba kubwa la kifahari lililozungukwa na ukuta mkubwa.
“ Wow ! inaonekana wazazi wake ni watu wenye kujiweza sana kiuchumi” akasema Mathew
“ Ndiyo.Wanamiliki biashara kadhaa kubwa kubwa hapa mjini.Ni watu wenye kujiweza sana” akasema Jason huku wakishuka na kuelekea katika geti.Mathew akabonyeza kengele ya getini na mlinzi aliyekuwa amevaa sare za kampuni binafsi ya ulinzi akafungua mlango mdogo wa geti
“ Habari zenu jamani” akawasabahi
“ Habari zetu nzuri.Habari za hapa?
“ Za hapa nzuri.Niwasaidie nini? Akauliza Yule mlinzi
“ Tuna hitaji kuonana na mzee Robinson Kobe”
“ Mzee si rahisi kumpata mida hii.Yuko katika shughuli zake.”
“ Vipi kuhusu mama? Yeye tunaweza kumpata? Akauliza Mathew
“ Hata mama naye ametoka “
“ Unaweza kutuelekeza mahala tunakoweza kumpata mama au mzee?
“ naweza kuwaelekeza ofisi ya mama ilipo lakini mzee ni mtu mwenye mizunguko mingi sana na kumpata si rahisi hata kidogo” akasema mlinzi na kuwaelekeza katika ofisi ya Bi Hellen Kobe mama wa Edson.Bila kupoteza muda Mathew na Jason wakaingia garini na kuelekea Kobe Shopping mall ambao ndiko iliko ofisi ya Bi Hellen.
Waliwasili Kobe’s shopping mall wakaegesha gari na kushuka wakaingia ndani ya jengo.Watu walikuwa wengi sana wakifanya manunuzi ndani ya jengo hili lililokuwa na biashara nyingi ndani yake
Kwa kutumia Lifti wakapanda hadi ghorofa ya tano iliko ofisi ya Bi Hellen Kobe mama wa Edson
“ Sina hakika kama Bi Hellen atakubali kuongea nasi endapo ataniona” akasema Jason
“ Kwa nini? Akauliza Mathew
“ Ananifahamu .Tumekuwa tukionana mahakamani wakati wa kesi na ananifahamu mimi ndiye wakili niliyemtetea mtuhumiwa wanayeamini kwamba ndiye alimuua mtoto wao.Lazima atakuwa na hasira nami” akasema Jason
“ Usijali Jason.Ataongea tu” akasema Mathew kwa kujiamini
Kabla ya kuingia katika ofisi ya Bi Hellen Kobe iliwalazimu waonane kwanza na katibu muhtasi wake ambaye aliwasiliana naye na kuwaruhusu waingie wakaonane naye.Wakati wakiingia ndani ya ofisi Bi Hellen,alikuwa anaongea na simu na mara tu alipokutanisha macho na Jason,mkono wa simu ukamponyoka na kuanguka mezani.Alistuka sana.
“ Ouh my gosh ! This is unbelievable !!..akasema Bi Hellen
“ You again….!!..Umeamua kunifuata hadi huku..!! akafoka Bi Hellen
Jason na Mathew hawakusema kitu wakaingia mle ofisini na kusimama mbele ya meza.
“ Shikamoo mama” akasema Mathew.Bi Hellen hakujibu kitu akainua mkono wa simu na kumpigia katibu muhtasi wake
“ Irene naomba tafadhali watoe watu hawa ofisini kwangu haraka sana.” Akasema kwa ukali Bi Hellen.Mathew akamnong’oneza kitu Jason ,akatoka mle ofisini.Bado Bi Hellen aliendelea kumuangalia Mathew kwa jicho kali hata baada ya Jason kutoka.Katibu muhtasi wa Bi Hellen akaingia mle ndani kwa ajili ya kumtoa Mathew ,huku akitabasamu Mathew akamwambia
“ Its ok Irene.Nina maongezi kidogo na mama ya muhimu sana.Naomba dakika tatu halafu nitatoka.We’re not here for trouble” Irene akamtazama Bi Hellen ambaye alimtazama Mathew usoni kwa sekunde kadhaa halafu akamfanyia ishara aketi kitini.
“ mama naomba nikusalimu tena shikamoo” akasema Mathew baada ya kuketi
“ Marahaba kijana.Una shida gani manake Yule mwenzako tayari amekwisha niharibia siku yangu.Simpendi na sitaki hata kumtia machoni”
“ Mama utanisamehe kwa kuongozana naye lakini ilinilazimu kufanya hivyo kwa sababu jambo lililonileta hapa hata yeye linamhusu vile vile” akasema Mathew
“ Ni jambo gani hilo lililowaleta? Akauliza Bi Hellen
“ Ni kuhusiana na mwanao Edson”
Bi Hellen akastuka kidogo
“ Edson?!
“ Ndiyo mama”
“ Unataka kunieleza nini kuhusu Edson?
“ Mama ,mimi naitwa Mathew ni mtu ninayefanya kazi za kiuchunguzi na kwa sasa ninafanya uchunguzi kuhusiana na kifo cha mwanao Edson” akasema Mathew
Bi Hellen akavuta pumzi ndefu ,akaweka kalamu yake mezani na kusema
“ Sikuelewi una maanisha nini unaposema unafanya uchunguzi wa kifo cha mwanangu.Tayari uchunguzi ulikwisha fanyika na muuaji akapatikana,akapandishwa kizimbani lakini kwa sababu wanazozijua wao mahakama ikamuachia huru,sasa unanishangaza unaposema kwamba unafanya uchunguzi wa kifo cha Edson” akasema Bi Hellen
“ Mama ,ninatamani sana tuongee jambo hili kwa upana wake lakini hapa si mahala pake.Naomba kama utakuwa tayari tuonane jioni ya leo nyumbani kwako ukiwa wewe na mzee na tutaongea kwa kina kuhusiana na jambo hili” akasema Mathew
“Mathew naona unanipotezea muda wangu wa kufanya kazi.Hakuna haja ya kufanya uchunguzi tena wakati kila kitu kiko wazi na muuaji alikwisha patikana lakini akaachiwa huru.Sisi tumekwisha muachia Mungu”
Mathew akamtazama Bi Hellen kwa makini na kusema
“ Mama ,mtu mnayeamini kwamba ndiye aliyemuua mwanenu siye.Peniela hakumuua Edson” akasema Mathew huku akiinuka.
“ Saa moja jioni ya leo nitakuja kuzungumza nanyi.Hakikisha mzee naye yupo ili tuzungumze sote kwa pamoja” akasema Mathew na kuondoka.Moja kwa moja akaelekea mahala walikoegesha gari ambako alimkuta Jason akimsubiri garini
“ Nilifahamu toka mwanzo Yule mama asingekubali kuongea nasi pindi akiniona.She hates me” akasema Jason
“ Usijali Jason.Jukumu letu ni kuwahakikishia kwa vitendo kwamba Penny hakumuua kijana wao.Si rahisi kukuamini kwa sasa lakini itafika wakati ambao wataamini tu. Jason nipeleke nyumbani kwa Penny” akasema Mathew.
“ Nyumbani kwa penny? Jason akashangaa kidogo
“ Yah ! nataka kwenda nyumbani kwa Penny”
“ Penny hayupo nyumbani kwake na hakuna anayeelewa yuko wapi”
“ Usijali Jason.Take me there” akasema Mathew huku akiendelea kuipekua kompyuta yake ndogo.
Baada ya Mathew kutoka mle ofisini ,Bi Hellen alimuita katibu muhtasi wake na kumuomba ampatie dawa zake kwani tayari alianza kujisikia vibaya.Maneno aliyoambiwa na Mathew yalimchanganya sana.
“ Yule kijana ni nani? Akawaza
“ Nani kamtuma afanye uchunguzi huo wakati uchunguzi wa awali ulikwisha fanyika na muuaji akapatikana? Kwa nini aliongozana na Yule wakili aliyemtetea muuaji wa mwanangu? Akawazza Bi Hellen akiwa amekiegemeza kichwa chake kitini.Hakujisikia tena kutaka kufanya kazi yoyote
“ No! hakuna mtu mwingine aliyemuua mwanangu zaidi ya Yule kahaba Peniela.Yeye ndiye aliyekutwa eneo la tukio na kuna kila ushahidi unaoonyesha kwamba ndiye aliyermuua Edson.Simuelewi huyu kijana anaposema kwamba anataka kufanya uachunguzi wakati uchunguzi ulikwisha fanyika na Mahakama ikamuachia mtuhumiwa” akaendelea kuwaza Bi Hellen na kuhisi mwili wake kuanza kutokwa na jasho jingi,akamuita dereva wake na kumuomba amrejeshe nyumbani
“ Yule kijana Mathew amenichanganya sana.Nashindwa nimuamini ama vipi.Amekitonesha kidonda changu kinachojaribu kupona” akawaza Bi Hellen akiwa garini kurejea nyumbani
*********
Jason na Mathew waliwasili nyumbani kwa Peniela.
“ Nisubiri humu humu garini” akasema Mathew huku akivaa glovu na kushuka akaenda getini,akatoa kidude Fulani toka katika koti lake na kulifungua kufuli lililofungiwa mlango mdogo wa geti akaufungua na kuingia ndani.
“ Huyu Mathew anaenda kufanya nini nyumbani kwa Penny wakati mwenyewe hayupo? Itakuaje iwapo Penny atagundua kwamba tumeingia ndani mwake wakati hayupo? Nina hakika akigundua hilo hataniamini tena na kuna hatari hata ukaribu mimi na yeye utapungua. I cant let that happen kwa sababu nina mipango mikubwa kuhusu Penny. Sijapendezwa na namna anavyoifanya kazi yake huyu jamaa” akawaza Jason akiwa garini
Ukuta ulioizunguka nyumba ya Peniela uliwekwa vipande vidogo vidogo vya chupa kwa juu.Mathew akapanda juu ya pipa tupu na kuweka kidude Fulani kati kati ya chupa zile akashuka na kuelekea katika majani mazuri yaliyooteshwa mbele ya nyumba ile ,akaufungua mkoba wake na kutoa kitu fulani mfano wa kipepeo akakibonyeza na kukirusha katikati ya majani yale.Yeyote ambaye angekiona angejua moja kwa moja yule ni kipepeo halisi. Kisha maliza kuviweka vitu vile akatoka akafunga geti na kurejea garini.
“ We can go now” akasema Mathew.Jason akavuta pumzi ndefu na kuliondoa gari maeneo yale.
*********
Katika jengo moja pembeni kidogo ya jiji la Dare s salaam,watu nane wameizunguka meza kubwa ya duara.Ni saa ya pili sasa wako katika kikao kizito.Mtu mmoja mwembamba mrefu ambaye uso wake ulikuwa umekunjana kwa hasira alikuwa akiongea kwa sauti kubwa
“Narudia kusema kwamba sitauvumilia tena uzembe kama huu mlioufanya.Haiwezekani siku ya pili leo msijue mahala aliko Penny.Amekwenda wapi? Mmempoteza vipi katika mitambo yenu wakati mlipaswa kumfuatilia saa ishirini na nne ? Naomba nirudie tena kuwaweka wazi kwamba Peniela ndiye dira yetu. Bila yeye hakuna kitu kinachoweza kufanyika.Operesheni 26B haiwezi kufanikiwa bila yeye.Kwa mwaka mzima ambao alikuwa gerezani akituhumiwa kila kitu kilisimama,na kwa sasa wakati amerejea na kila kitu kimeanza kwenda upya mnafanya tena uzembe.Ninaapa kwa mbingu na nchi kwamba sintouvuilia uzembe wa aina yoyote ile kuanzia sasa.Peniela anatakiwa afuatiliwe kwa saa ishirini na nne. Hamtakiwi kumuacha hata dakika moja.Nawaweka wazi kwamba endapo operesheni 26B itashindwa kufanikiwa kwa sababu ya uzembe tu wa watu basi tujihesabu sisi sote ni marehemu.I want to live,I don’t want to die so I cant lost my soul because of one stupid.If you mess again you’ll die first” akasema kwa ukali Yule jamaa.Watu wote walikuwa kimya wakimsikiliza na walionekana kuingiwa na woga mwingi.Kijana mmoja aliyevalia suti nyeusi na shati jekundu akakohoa kidogo na kusema
“Captain,tulijitahidi kumfuatilia Penny kwa karibu lakini kifaa ambacho huwa anatumia kwa ajili ya mawasiliano nasi kilizimwa usiku wa manane.Tulipokwenda asubuhi nyumbani kwake kufanya uchunguzi tulikutana na makufuli,Penny hakuwepo.Toka amemaliza kesi iliyokuwa ikimkabili Penny anaonekana hataki tena kushirikiana nasi.Hatoi ushirikiano wa aina yoyote.Sina hakika kama yuko tayari kuendelea na operesheni hii” akasema Yule kijana na kumfanya Captain agonge meza kwa hasira
“ Kwa nini mlienda asubuhi?? Ilitakiwa muda ule ule ambao mmeona tukio lile la kukatika kwa mawasiliano mngenitaarifu mara moja ili nijue nini cha kufanya.Uzembe wenu unatugharimu sisi sote.Narudia tena kwamba hili ni onyo la mwisho.Kuhusu Penny kutotoa ushirikiano hilo niachieni mimi.Atake asitake lazima afanye tunavyotaka sisi na si vinginevyo.” Akanyamaza kidogo halafu akaendelea
“ Leo usiku nina kikao na wakuu cha kujadili kuhusu operesheni 26B ambayo inatakiwa kuzinduliwa rasmi upya.Kabla sijaelekea kikaoni usiku wa leo nahitaji kupata taarifa kwamba tayari mmekwisha fahamu mahala alipo Penny.Kuanzia sasa nendeni tena katika vifaa vyenu,fungueni kompyuta zenu,nendeni katika satellite na mjue wapi aliko Penny.Mna kila kitu kinachotakiwa kwa hiyo ifanyeni kazi na kabla ya saa mbili usiku wa leo nataka ripoti.” Akasema kwa ukali Captain na kutoka mle katika chumba cha mikutano akaingia ofisini kwake akajifungia.Alihisi kichwa kizito kwa mawazo.
TUKUTANE TENA SEHEMU IJAYO……SEASON 1
SEHEMU YA 14
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ Kwa nini mlienda asubuhi?? Ilitakiwa muda ule ule ambao mmeona tukio lile la kukatika kwa mawasiliano mngenitaarifu mara moja ili nijue nini cha kufanya.Uzembe wenu unatugharimu sisi sote.Narudia tena kwamba hili ni onyo la mwisho.Kuhusu Penny kutotoa ushirikiano hilo niachieni mimi.Atake asitake lazima afanye tunavyotaka sisi na si vinginevyo.” Akanyamaza kidogo halafu akaendelea
“ Leo usiku nina kikao na wakuu cha kujadili kuhusu operesheni 26B ambayo inatakiwa kuzinduliwa rasmi upya.Kabla sijaelekea kikaoni usiku wa leo nahitaji kupata taarifa kwamba tayari mmekwisha fahamu mahala alipo Penny.Kuanzia sasa nendeni tena katika vifaa vyenu,fungueni kompyuta zenu,nendeni katika satellite na mjue wapi aliko Penny.Mna kila kitu kinachotakiwa kwa hiyo ifanyeni kazi na kabla ya saa mbili usiku wa leo nataka ripoti.” Akasema kwa ukali Captain na kutoka mle katika chumba cha mikutano akaingia ofisini kwake akajifungia.Alihisi kichwa kizito kwa mawazo.
ENDELEA…………………………………
Saa moja kasoro dakika nane za jioni,Mathew alisimamisha gari nje ya nyumba ya Bwana na Bi Robinson Kobe wazazi wa Edson.Jioni hii alikuwa ameambatana pia na wakili Jason.Geti lilifunguliwa wakaingia ndani
“ Mathew una hakika watakubali kuongea nasi wakiniona nimeongozana nawe? Akauliza Jason kwa wasi wasi
“ Usijali Jason.Wataongea nasi tu” akasema Mathew huku akibonyeza kengele ya mlango wa sebuleni ambao ulifunguliwa na mwanadada mmoja mwembamba mrefu.Aliwakaribisha sebuleni na kuwahudumiwa vinywaji na baada ya dakika kama tatu hivi wazazi wa Edson wakatokea.Bi Hellen alikuwa anatembea kwa uchovu na ilionekana wazi kwamba hali yake haikuwa nzuri.Hii ilitokana na mstuko alioupata mchana baada ya kuongea na Mathew na kumkumbusha kuhusiana na kifo cha mwanae Edson .Jason na Mathew wakasimama na kuwasalimu wazee wale kwa heshima .Bado Bi Hellen aliendelea kumuangalia Jason kwa macho makali sana .Ilionyesha wazi kwamba hakupendezwa na uwepo wake pale
“ Karibuni vijana” akasema mzee Robinson Kobe
“Nimeambiwa kwamba mna jambo mnataka kuzungumza nasi”
“ Ndiyo mzee.Tulionana na mama mchana na tukaomba tukutane na kuonana nanyi.Tuna jambo tunataka kuzungumza nanyi wazee wetu” akasema Mathew
“ Ni kuhusu nini? Akauliza mzee Robinson
“ Ni kuhusu mwanetu Edson”
“ Kuna jambo gani kumuhusu Edson? Kesi yake imekwisha malizika na mtuhumiwa akaachiwa huru.Huyo mwenzako anafahamu kila kitu kwani yeye ndiye aliyekuwa akimtetea mtuhumiwa” akasema mzee Robinson
“ Nalifahamu hilo mzee” akasema Mathew na kunyamaza kidogo kisha akaendelea
“ Wazee wangu naomba kwanza nijitambulishe kwenu kwa sababu huyu mwenzangu tayari mnamfahamu.Mimi naitwa Mathew Kwanga.Kazi yangu ni mchunguzi wa kimataifa.Ninapokea na kufanya kazi mbali mbali za kiuchunguzi toka sehemu mbali mbali duniani” akanyamaza kidogo na kuendelea
“ Nilifuatwa na ndugu zangu hawa wawili.Jason na mwingine ambaye tulitakiwa kuwa naye hapa lakini amepata udhuru .Yeye ni Jaji Elibariki ambaye alikuwa akiisikiliza kesi ya mauaji ya Edson.” Akasema Mathew.Wazazi wa Edson wakatazamana baada ya jina la Jaji Elibariki kutajwa
“ Ndugu zangu hawa “ akaendelea Mathew
“ Waliniomba niwasaidie kufanya uchunguzi kuhusiana na kifo chenye utata cha kijana wenu Edson na kumfahamu nani muuaji”
Kabla hajaendelea mzee Robinson akaingilia kati
“ Kijana Uchunguzi ulikwisha fanyika na mtuhumiwa akapatikana japokuwa mahakama kwa sababu wanazozijua wao wakamuachia huru. Sioni haja ya kufanya tena uchunguzi kwa sababu jambo hili sisi tumekwisha muachia Mungu kwani yeye pekee ndiye mwenye kutenda haki.Duniani hapa hakuna haki” akasema mzee Robinson akionekana kukata tamaa
Jason aliyekuwa kimya toka wamefika akakohoa kidogo na kusema
“ Mzee naomba na mimi niongee kidogo” akasema huku akitazamana na mzee Robinson.Akaendelea
“ Naomba niwafahamishe wazee wangu kwamba Peniela siye muuaji wa Edson?
Kauli ile ilimfanya mzee Robinson amtazame kwa jicho kali na kusema
“ Kijana ,nafahamu kwamba wewe ni mwanasheria mahiri kabisa na umeifanya kazi yako vyema ya kuishawishi mahakama ikakubali kumuachia huru mteja wako.Najua hata siku moja hutakubali kwamba mteja wako alimuua mwanetu.Yote hii ni kwa sababu anakulipa pesa nyingi.Pesa inaweza kufanya jambo lolote hata kupindisha sheria na wenye hatia wakaachiwa huru.Ndiyo maana hapo awali nilisema kwamba haki inapatikana mbinguni tu.Huku duniani hakuna haki.” Akasema mzee Robnson
“Hapana mzee.Si hivyo unavyofikiri.Sheria na Mahakama vimewekwa ili kutoa haki.Mahakama haiko kwa ajili ya kupindisha sheria na kulipendelea kundi fulani la watu kwa sababu ya pesa zao au nafasi zao.Peniela aliachiwa huru baada ya mahakama kuridhika kwamba hakuwa na hatia.Hakutenda kosa.Hakumuua Edson.Baada ya kesi kumalizika na Peniela kuachiwa huru ,Jaji Elibariki ambaye ndiye aliyetoa hukumu ile alinifuata na kunieleza nia yake ya kufanya uchunguzi wa kina kuhusiana na kifo cha Edson.Aliamua kufanya hivyo kutokana na sintofahamu nyingi alizozigundua katika mwenendo mzima wa kesi ile.” Jason akanyamaza kidogo na kusema
“ Kumekuwa na maneno mengi na hisia tofauti kuhusiana na hukumu ile kwa hiyo tunataka tufanye uchunguzi wa kina tuufahamu ukweli.Tumfahamu muuaji wa edson na kumfikisha sehemu husika apate adhabu stahili.Kwa kuwa sisi ni wanasheria na hatuna taaluma ya kiuchunguzi tumeamua kutumia gharama zetu kumkodisha huyu ndugu yetu Mathew aweze kuifanya kazi hiyo.Yeye amebobea katika masuala haya ya kiuchunguzi,amekwisha fanya kazi katika idara mbali mbali nyeti za kiusalama hapa nchini kabla ya kuamua kufanya kazi zake binafsi.Kabla ya kuanza kufanya uchunguzi wake Mathew ameona ni bora aje azungumze nanyi mambo kadhaa. “ akasema Jason.Kimya kikatawala pale sebuleni.Mzee Robinson aliinama akatafakari huku akikuna kichwa chake.Baada ya dakika mbili akainua kichwa na kusema
“Natamani niamini maneno uliyoniambia kijana wangu lakini nafsi yangu inakataa kabisa. Sidhani kama kuna kitu cha kunishawishi niamnini kwamba Penny siye aliyemua mwanangu” akasema mzee Robinson
“ Mzee wangu sina kitu cha kukushawishi kwa sasa lakini naomba unipe muda kidogo tu na nitakuwa na cha kukukushawishi uamini hivyo.Ninachohitaji toka kwenu sasa ni ushirikiano tu” akasema Mathew.Mzee Robinson akainama akafikiri na kusema
“ Unahitaji nini toka kwetu?
“ Mzee,mimi ni mzoefu katika masuala haya .Nimekwisha fanya chunguzi mbali mbali za vifo vyenye utata kama hiki cha mwanao.Mara nyingi kinapotokea kifo kama hiki kunakuwa na sababu Fulani nyuma yake.Sitaki kuongea sana lakini ninachotaka kukisema ni kwamba tutaifahamu sababu hiyo na kwa nini Edson aliuawa.Sahauni uchunguzi uliopita na tushirikiane katika uchunguzi huu tunaotaka kuufanya. Kitu cha kwanza ninachotaka kukifahamu toka kwenu japo kwa ufupi tu ni kuhusiana na mwanenu Edson alikuwa ni mtu wa namna gani?
Mzee Robinson akavuta pumzi ndefu na kusema
“ Edson alikuwa ni mtoto pekee wa kiume kati ya watoto wanne tulionao.Kimakuzi Edson tumemlea katika maadili mazuri.Alikuwa ni kijana mtaratibu sana na asiye na makuu.Alipohitimu shahada yake ya mawasiliano nchini marekani alirudi nchini na akapata kazi katika kampuni moja ya simu na baadae akapata kazi ikulu katika kitengo cha mawasiliano ambako alifanya kazi hadi mauti yalipomkuta.Kitabia Edson hakuwa na tabia ambayo naweza kusema kwamba ni mbaya,hakuwa mnywaji wa pombe ,wala mtumiaji wa kilevi chochote kile.Muda mwingi aliutumia kwa kusoma na kufanya kazi zake.Alipoanza kazi ikulu alianzisha mahusiano na kimapenzi na Anna binti wa rais.Urafiki wao ulianza toka wakiwa wadogo kwa sababu familia zetu mbili ni familia rafiki kwa muda mrefu sana.Baada ya kuingia katika mahusiano na Anna,tuliamua kumpatia moja ya nyumba zetu aishi ili aweze kuwa huru.Edson na Anna walipendana sana na sote tulikuwa na matarajio makubwa kwamba siku moja familia zetu mbili zingeweza kuunganishwa na hawa vijana lakini ghafla tukasikia kwamba wamefarakana na tayari Edson alikuwa katika mahusiano na msichana mwingine aitwaye Peniela.Hatukutaka kuingilia mambo yake ya kimahusiano tukamuacha aendelee na Peniela hadi pale mauti yalipomkuta.Kwa ufupi hivyo ndivyo ninavyoweza kumuelezea mwanangu Edson japokuwa kuna mambo mengi sana ambayo naweza kuyaeleza. Kuhusiana naye” akasema mzee Robinson
“ I see….He was a nice guy..” akasema Mathew
“ Yah ! ..” akajibu mzee Robinson
“ Siku chache kabla ya kifo chake ulifanikiwa kuonana naye? Alikuwa katika hali gani? Kuna kitu chochote ambacho hakikuwa cha kawaida kwa namna ulivyomuona? Akauliza Mathew.Mzee Robinson akafikiri kidogo na kusema
“ Nilionana naye wiki mbili kabla ya kifo chake.Alikuja ofisini kwangu tukaongea kidogo akaondoka.Alikuwa katika hali ya kawaida kabisa.Ninachokumbuka ni siku tatu kabla ya kifo chake alimpigia simu mama yake usiku na kuongea naye.Alikuwa anamsalimu tu.Hakuwa na kawaida ya kupiga simu usiku lakini hakusema kama ana tatizo lolote ” akasema mzee Robinson
“ Nilifika katika nyumba aliyokuwa akiishi Edson nikaambiwa kwamba umeiuza” akasema Mathew
“ Ndiyo niliamua kuiuza ile nyumba. Sikutaka kuendelea kuimiliki ile nyumba baada ya mwanangu kuuliwa ndani yake” akasema mzee Robinson
“ Vifaa vyake mmevihifadhi wapi? Akauliza Mathew
“ Tuna nyumba ndogo iko huko nyuma ndiko tumevihifadhi”
“ Nitahitaji kuvipitia baadhi ya vitu vyake kama vitabu vya kumbu kumbu ili tuonne kama kuna kumbu kumbu yoyote isiyo ya kawaida ambayo anaweza kuwa aliiweka vitabuni ,vile vile kompyuta yake pamoja na simu” akasema Mathew
“ Edson alikuwa na vitabu vingi sana kwani alikuwa msomaji mzuri.Nadhani tunaweza kuchukua siku kadhaa kuvipitia vyote kuchambua kimoja kimoja.Kuhusu kompyuta zake ni kwamba hazikuwahi kuonekana na hatujui ni nani aliyezichukua.Simu yake pia haikuwahi kuonekana.Hatuelewi ni kwa nini vitu hivi vilitoweka katika mazingira yenye utata mkubwa. Akasema mzee Robinson
“ Baba Eddy..! akaita Bi Hellen
“ Kuna kitu nimekikumbuka.Katika mojawapo ya chungu cha maua kilichokuwa chumbani kwake siku tunahamisha vyombo vyake ilianguka laini ya simu ambayo nimeihifadhi ndani.Nadhani inaweza ikawa ni ile laini ya simu ambayo aliitumia aliponipigia simu mara ya mwisho kwa sababu hakutumia namba zake ninazozifahamu.” akasema Bi Hellen
“ Ok,nitaomba unipatie laini hiyo ya simu ili tuifanyie uchunguzi.Inaweza ikawa na jambo la muhimu kwetu” akasema Mathew na Bi Hellen akainuka akaelekea chumbani kuchukua laini ile ya simu
“ Bado sijapata jibu ni kwa nini muuaji aliondoka na kompyuta na simu wakati Edson alikuwa na kiasi cha shilingi milioni ishirini ndani.” Akasema mzee Robinson
“ Shida yao haikuwa pesa.Kuna kitu walichokuwa wakikitafuta ambacho ni zaidi ya pesa” akasema Mathew
“ Kwa mbali hata mimi ninaanza kupata picha kwamba mauaji ya kijana wangu ni tofauti kabisa na tunavyofikiri.Yawezekana kuna mtu au kitundi cha watu waliofanya mauaji yale na si Yule msichana aliyekuwa akituhumiwa” akasema mzee Robinson.Mathew na Jason wakatazamana.
“ Ahsante sana mzee kwa kuliona hilo.Jukumu letu sasa ni kubaini mtu huyo au kikundi cha watu waliotekeleza mauaji hayo “ akasema Mathew .Bi Helen akarejea na kumpatia ile laini ya simu aliyoikuta katika vifaa vya Edson
“ Wazee wangu nashukuru kwa kutusikiliza .Mimi na wenzangu tutafanya kila tuwezalo kuhakikisha kwamba tunaufahamu ukweli.Nitakuwa nikiwapa taarifa za mara kwa mara kuhusiana na uchunguzi wetu unavyoendelea .Ninachoomba suala hili liwe ni la siri na asifahamu mtu mwingine yeyote kwamba kuna uchunguzi unaendelea .” akasema Mathew
“ Msijali vijana wangu,muda wowote mnakaribishwa.Hapa ni nyumbani kwenu na milango iko wazi muda wote.Chochote mnachokihitaji msisite kutueleza tuwasaidie.” Akasema mzee Robinson
“ Tunashukuru sana wazee wetu.Sisi tutajitahidi kwa kila tuwezavyo kuhakikisha tumelichimba suala hili hadi katika mzizi wake na tuufahamu ukweli.Endapo kuna chochote kile mnaachoona kinaweza kutusaidia katika uchunguzi wetu msisite kututaarifu” akasema Mathew. Wakaagana na kuondoka.
“ Tayari kuna mwanga umeanza kuonekana,” akasema Mathew
“ kuna sababu iliyowafanya watu watu waliofanya mauaji ya Edson waondoke na kompyuta zake na simu.Kuna kitu gani walikuwa wanakificha? Kwa kuwa Edson alikuwa katika masuala ya mawasiliano inawezekana kuna jambo alikuwa analifahamu ambalo hakupaswa kulifahamu na kusababaisha kifo chake.Tutajua tu ni jambo gani hilo” akasema Mathew.Jason akaitika kwa kichwa alikuwa kimya sana .Mawazo yake yote yalikuwa kwa Peniela.Alijiuliza maswali mengi mahala aliko na kwa nini ameizima siku yake
“ Baba Eddy !.. akaita Bi Hellen baada ya Mathew na Jason kuondoka
“ Niliwadharau wale vijana lakini wamenifumbua macho na kwa sasa hata mimi nimeanza kuamini kwamba kuna watu walimuua mwanangu kwa sababu maalum ingawa itanichukua muda mrefu kuamini kwamba Yule msichana Peniela hakuhusika na kifo cha Edson” akasema bi Hellen.Mzee Robinson akavuta pumzi ndefu na kusema
“ Peniela hakumuua Edson” akageuka na kujifunika shuka akalala mke wake akabaki akimshangaa
*********
Jason alimfikisha Mathew nyumbani kwake na kisha akaendelea na safari ya kuelekea kwake.Mathew akaingia ndani mwake na kitu cha kwanza alichokifanya ni kuelekea katika chumba chake kikubwa kilichokuwa na runinga kubwa nane zilizotundikwa ukutani.Akaziwasha runinga zote na zikaanza kuonyesha picha zikaanza kuonekana.
“ wow ! my birds are working” akasema na kukaa kitini akaanza kufuatilia picha zile zilizokuwa zikionekana katika runinga.Runinga namba sita ilikuwa ikionyesha makazi ya Peniela.Vifaa vile mithili ya vipepeo Mathew alivyoviweka katika nyumba ya Peniela mchana vilikuwa ni kamera ambazo zilikuwa zikionyesha kila kilichokuwa kikiendelea katika makazi yale.Alizipeleka mbele picha zile na hakukuonekana mtu yeyote akiingia katika makazi yale hadi ilipotimu saa mbili na dakika ishirini na mbili.Geti dogo lilifunguliwa na watu wawili wakaingia kwa kunyata huku wakiwa na bastora mikononi.
“ Who are these people? Akajiuliza Mathew huku akiisogelea karibu runinga yake.
TUKUTANE TENA SEHEMU IJAYO……SEHEMU YA 15
ILIPISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Jason alimfikisha Mathew nyumbani kwake na kisha akaendelea na safari ya kuelekea kwake.Mathew akaingia ndani mwake na kitu cha kwanza alichokifanya ni kuelekea katika chumba chake kikubwa kilichokuwa na runinga kubwa nane zilizotundikwa ukuitani.Akaziwasha runinga zote na zikaanza kuonyesha picha zikaanza kuonekana.
“ wow ! my birds are working” akasema na kukaa kitini akaanza kufuatilia picha zile zilizokuwa zikionekana katika runinga.Runinga namba sita ilikuwa ikionyesha makazi ya Peniela.Vifaa vile mithili ya vipepeo Mathew alivyoviweka katika nyumba ya Peniela vilikuwa ni kamera ambazo zilikuwa zikionyesha kila kilichokuwa kikiendelea katika makazi yale.Alizipeleka mbele picha zile na hakukuonekana mtu yeyote akiingia katika makazi yale hadi ilipotuimu saa mbili na dakika ishirni na mbili.Geti dogo lilifunguliwa na watu wawili wakaingia kwa kunyata huku akiwa na bastora mikononi.
“ Who are these people? Akajiuliza Mathew huku akiisogelea karibu runinga yake.
ENDELEA………………………………
Watu wale wawili walikuwa makini sana wakiangaza huku na huko halafu wakaweka kitu Fulani kidogo katika mlango wa kuingilia sebuleni kwa Penny.
“ Wanaweka nini pale? Akajiuliza Mathew na kuikuza picha ili aone kitu kile kilichokuwa kimewekwa pale mlangoni.
“ Kamera !..” akasema kwa sauti ndogo
“ Wameweka kamera .Kwa nini wameweka kamera mlangoni? These people looks so professional” akawaza Mathew.
Baada ya kuweka kamera ile mlangoni kwa Peniela,kwa kutumia vifaa maalum wakafungua mlango wakaingia ndani.Mathew hakuweza kuona kilichokuwa kinaendelea ndani kwa sababu hakuwa ametega kamera yoyote ndani ya nyumba ya Penny.Baada ya kama dakika kumi hivi watu wale wakatoka na kuondoka na kuzidi kumchanganya Mathew
“ Watu wale ni akina nani? Wamefuata nini kwa Peniela? Akaendelea kujiuliza Mathew.Akarudisha tena picha nyuma na kuwatazama vizuri watu wale
“ Watu hawa ni akina nani ? kwa nini wameweka kamera mlangoni kwa Penny.Mle ndani waliingia kufanya nini? Akawaza huku akiendelea kuwatazama wale wale jamaa katika runinga.
“ Hapa kuna jambo ambalo si la kawaida.Watu hawa wamekuja wakiwa na bastora mkononi na tena wanaonekana ni watu makini na wazoefu.Mhh! suala hili si dogo kama ninavyolifikiri.Tayari nimepata sehemu ya pili ya kufanyia uchuguzi .Natakiwa kuwafahamu watu hawa ni akaina nani, na nini lengo la kuja kwa Peniela wakati mwenyewe hayupo.” Akawaza Mathew na kuprint zile picha za wale jamaa.
“Bado sipati jibu watu wale ni akina nani na kwa nini wameweka kamera nyumbani kwa Penny.Nadhani lengo lao ni kufuatilia kila kinachoendela pale. Inaonekana kuna watu ambao wanafuatilia nyendo za Penny na walifahamu fika kwamba kwa muda huu hayupo nyumbani ndiyo maana wakaingia na kufanya walichotaka kukifanya.Watu hawa lazima niwafahamu na nini lengo lao kwa Penny.Ninaanza kuwa na wasi wasi sana kuhusiana na maisha ya Penny.Inaonekana yuko katika hatari kubwa.Kuna watu wanaomfuatilia ambao sijui lengo lao ni nini .Penny yuko wapi? Kwa mujibu wa Jason ni kwamba siku ya pili leo Penny hajulikani yuko wapi .Kesho nitaanzia kazi kwa Penny.Lazima nifahamu yuko wapi ” Akawaza Mathew na kuondolewa katika mawazo na simu iliyoita.Zilikuwa ni namba ngeni katika simu yake
“ Hallow ! akasema
“ Hallow kaka,kuna mtu anahitaji kuongea nawe.” Ikasema sauti ya upande wa pili.Baada ya sekunde kadhaa akasikia sauti tamu ambayo aliitambua mara moja
“ Hallo Mathew” ikasema sauti ile
“ Anitha ! akasema Mathew
“ Niko hapa uwanja wa ndege wa Julius Nyerere”
“ Ouh gosh ! Kwa nini hukuniambia utaingia muda gani ili nije nikupokee?
“ Hapana sikutaka kukusumbua Mathew.Hapa ni nyumbani.Nisubiri hapo hapo nyumbani nitachukua taksi” akasema Anitha na kukata simu
“ The hacker is here…” akasema Mathew kwa sauti ndogo huku akitabasamu.
“ Bado Noah.yeye aliniambia anakuja kesho.Kazi imeiva” akawaza Mathew huku akiendelea kuziangalia picha mbali mbali zilizokuwa zinapita katika runinga zilizokuwamo mle ndani.
**********
Penny alijiangalia katika kioo kikubwa ,kugeuka nyuma akajitazama na kutabasamu
“ Siku zote huwa sina wasi wasi na uzuri wangu” akasema Penny kwa sauti ndogo huku akiikoleza rangi ya mdomo.Akachukua kichupa kidogo cha uturi na kudondoshea matone machache shingoni.
“ Leo lazima Dr Joshua atapagawa na mimi.Ni muda mrefu sana hajakutana nami.Nitampa vitu adimu ambavyo vitampagawisha na kumchanganya .Huu ni wakati wa kutumia kila aina ya ujuzi nilionao ili niweze kuimaliza kazi” akawaza Penny huku akichukua mkoba wake mdogo na kufungua mlango.Nje ya mlango wake alisimama kijana mmoja aliyevalia nadhifu.
“ Uko tayari? Akauliza Yule kijana
“ Ndiyo niko tayari.Tunaweza kwenda” akasema penny na kuongozana na Yule kijana mpaka katika gari moja la kifahari akafunguliwa mlango na kuingia kisha wakaondoka.
“ Najua Jason na Jaji Eklibariki watakuwa wamenitafuta sana baada ya kutoniona kwa siku ya pili leo.Natamani niwataarifu kwamba niko salama lakini naogopa kwani Kareem alinionya nisimpigie simu mtu yeyote na kumfahamisha kwamba niko Arusha.” Akawaza Penny akiwa garini
“ Sijui wamefikia wapi ule mpango wao wa kumtafuta muuaji wa Edson.Nikirudi nitawashauri waachane na jambo hili kwani lina mkanganyiko mkubwa na ni hatari kwa usalama wao.Sitaki yeyote kati yao apatwe na tatizo lolote.Hawa ni watu wangu wa muhimu sana bila wao hivi sasa ningekuwa ninakula maharage ya jela. ” Akaendelea kuwaza na mara picha ya Jason ikamjia kichwani .
Saa tatu na dakika arobaini wakawasili Meru view hotel,moja kati ya hoteli kubwa sana afrika mashariki na kati.Ni katika hoteli hii ndipo alipofikia rais wa jamhuri ya mungano wa Tanzania Dr Joshua tayari kabisa kwa ajili ya kuongoza kikao cha wakuu wa nchi za afrika msahariki kinachotarajiwa kufanyika jijini Arusha kwa muda wa siku tatu.Ulinzi ulikuwa mkali sana kuizuguka hoteli hii na kila gari lililoingia hapa ililazimika kukaguliwa na askari.Gari alilopanda Penny halikukaguliwa likapita moja kwa moja hadi katika maegesho ya viongozi wakuu mlango ukafunguliwa na Penny akashuka.
“ Wow ! what a beautiful place” akawaza Penny huku akitabasamu akiifurahia mandhari ile ya kupendeza ya hoteli ile kubwa.Yule kijana ambaye hakuwa muongeaji alimuongoza Penny hadi katika mlango wa nyuma wakaingia ndani ya hoteli na kwa kutumia lifti wakapanda hadi ghorofa ya sita wakashuka na kulifuata varanda refu.Hakukuwa na mtu anayeranda randa katika ghorofa hii zaidi ya walinzi wa rais ambao walikuwa makini na kila aliyeonekana eneo hili. Hakuna kati yao aliyethubutu kumuuliza chochote Penny kwani alikuwa ameongozana na mmoja wa walinzi wa rais.Moja kwa moja akampeleka Penny hadi katika chumba cha rais akagonga mlango ukafunguliwa na Kareem mlinzi wa rais.
“ Penny karibu ndani” akasema Kareem huku akimshika mkono na kumuelekeza aketi sofani.Kilikuwa ni chumba kikubwa na kizuri mno.Kwa muda wa sekunde kadhaa Kareem aliendelea kuchezea simu yake halafu akainua kichwa na kusema
“ Unatumia kinywaji gani Penny?
“ Nipatie mvinyo tafadhali” akasema Penny.Kareem akamletea chupa ya mvinyo na kumuwekea mezani
“ Mheshimiwa rais bado yuko katika kikao.Utaendelea kumsubiri” akasema Kareem na kuendelea kuchezea simu yake kubwa
“ How’ve u been Kareem? Maisha yako yanakwendaje? Akaamua kuanzisha maongezi Penny baada ya kuona Kareem amekuwa kimya sana na ilionyesha hakutaka maongezi
“ I’m ok Penny.I’m doing fine.Samahani kama umeboreka lakini niko kazini.Tuna marais karibu watano watahudhuria mkutano mkubwa wa marais wa afrika mashariki kuanzia kesho kwa hiyo yatubidi tuwe macho sana katika ulinzi ndiyo maana unaniona nimekuwa kimya sana nafuatili akila kinachoendelea hapa hotelini”
“ Usijali Kareem.Ninaelewa” akasema Penny na kuelekeza macho yake runingani akitazama muziki
“ Kareem ! akaita Penny baada ya muda
“ Unasemaje Penny? Akauliza Kareem
“ Nitakuwepo hapa Arusha kwa muda gani?
“ As long as present wants” akajibu Kareem, kwa ufupi
“ No Kareem.I need to go back to Dar as soon as possible.” Akasema Penny
Kareem hakumsemesha kitu akaendelea na kazi zake
Saa sita na dakina nane mlango wa chumba cha rais ukafunguliwa na Dr Joshua rais wa jamhuri ya muungano akaingia
“ Where is she? Akamuuliza Kareem ambaye alimfanyia ishara kwamba tayari yuko chumbani
“ Thank you Kareem.Thank you so much.From now I need a privacy.No calls no any disturbance” akasema Dr Joshua
“ Ok Mr President” akajibu Kareem kwa adabu.Dr Joshua akakinyonga kitasa cha mlango na kuingia chumbani kwake.Ilimlazimu avue miwani yake ili ajiridhishe kwamba alichokuwa akikiona kitandani binadamu wa kawaida na si malaika .Kiumbe kilichokuwa kimejilaza katika kitanda kilichotandikwa mashuka mazuri meupe kilikuwa na uzuri usio wa kawaida.
“ Penny ! akaita
“ Dr Joshua ! akasema Penny kwa sauti ndogo.Dr Joshua akafunga mlango na kumuendea Penny akamkumbatia kwa nguvu
“ Welcome back my angel” akasema Dr Joshua .Penny hakutaka kupoteza muda akammwagia mzee Yule mabusu mfululizo na kumchanganya. Dr Joshua akajikuta akianza kuhema kwa nguvu.Taratibu akatoa ulimi na kuuingiza kinywani kwa Dr Joshua ambaye alianza kutoa miguno.Penny akamvua koti taratibu huku akiendelea kumfanyia manjonjo yaliyozidi kumpagawisha Dr Joshua. Taratibu akalegeza tai na kuitoa halafu akaanza kufungua vifungo vya shati .Alikichezea kifua cha mzee yule kwa ufundi mkubwa halafu akaufungua mkanda wa suruali yake ikaanguka chini akabakiwa na nguo ya ndani,Penny akaivuta taratibu nguo ile ya ndani akaishusha hadi magotini halafu akapiga magoti na kuanza kufanya utundu maeneo ya ikulu.Dr Joshua hakuwa akijiweza tena.Penny akamsukuma akangukia kitandani halafu akafungua zipu ya gauni lake likaanguka chini.Dr Joshua mate yakamtoka alipoushuhudia mwili mwororo wa kimalaika wa msichana aliyesimama mbele yake.Taratibu akaivua nguo yake ya ndani na kupanda kitandani na kuendeleza utundu.Dr Joshua alibaki akilalama kwa raha alizokuwa akipewa.Baada ya dakika kumi na tano tayari walikuwa wakiogelea katika ulimwengu wenye raha isiyoelezeka.
*******
“ Ouh Peniela..nakosa neno la kusema kwa raha ulizonipa.I missed you .I missed this….” Akasema Dr Joshua akiwa hoi baada ya kumaliza mzunguko mmoja.Penny akajiinua na kumsogelea akambusu na kukilaza kichwa chake kifuani
“ I missed you too Dr Joshua..Umri umekwenda lakini bado una nguvu kama kijana wa miaka kumi na nane.You make me so happy” akasema Penny
“ Muda wote uliokaa gerezani ukikabiliwa na kesi nilikosa raha na amani.Kwa sasa najiona kijana tena.You are amazing my angel” akasema Dr Joshua huku akizichezea nywele za Penny
“ Don’t lie to me Dr Joshua.Kama ningekuwa na umuhimu kwako usingekubali kuniona nikiteseka gerezani mwaka mzima kwa kosa ambalo sikulitenda na zaidi ya yote ulishinikiza nifungwe kifungo kirefu gerezani.You didn’t stand by my side.Pamoja na mateso yote na hata kunusurika kwenda maisha gerezani lakini sikufumbua mdomo wangu na kuongea lolote kuhusiana na kifo cha Edson.Ninajua wewe ndiye uliyeamuru watu wako wamuue Edson kwa sababu unazozijua mwenyewe lakini kwa kuwa ninakupenda Dr Joshua mpaka leo hii hakuna mtu anayefahamu chochote” akasema Penny na machozi yakamtoka alipomkumbuka Edson.Dr Joshua akamfuta machozi na kusema
“ Tafadhali usilie Penny.Usilie malaika wangu.Kuna mambo mengi ambayo yametokea kitu cha kwanza ninachokihitaji toka kwako ni msamaha wako.Ni kweli nilikuacha ukaingia katika matatizo makubwa na sikusimama pamoja nawe.Penny please forgive me my angel.We have so many to talk” akasema Dr Joshua.Penny akainua kichwa akamtazama na kusema
“ Nimekwisha kusamehe Dr Joshua na ndiyo maana niko hapa.Umesema tuna mambo mengi ya kuongea hata mimi nina mengi ya kuuliza lakini kwanza nataka unieleze kwa nini Edson aliuawa? Akauliza Penny.Dr Joshua akachukua kitambaa na kujifuta jasho,akainuka na kwenda mezani akajimiminia mvinyo na kupiga funda kubwa.
TUKUTANE SEHEMU IJAYO…………