Klabu ya Azam FC imemtangaza kocha Youssouph Dabo raia wa Senegal kuwa kocha mkuu wa klabu hiyo kuanzia msimu ujao na amesaini mkataba wa miaka mitatu. Dabo ni kocha wa zamani wa klabu ya Tenguteh FC ya Senegal iliyofuzu makundi ya klabu bingwa Afrika msimu 2020/21 kwa kuitoa Raja Casablanca ya Morocco.
-Ila baada ya kauli hiyo Dabo alitangaza kuwa alishaachana na timu hiyo tangu mwanzoni mwa mwezi February na sababu kubwa ikitajwa ni kauli yake aliyoitoa kwenye bodi ya timu hiyo kwa kuwaambia mwishoni mwa msimu huu ataondoka kwenye klabu hiyo na kujiunga na moja klabu nchini Tanzania
